Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Jerry Sabi akiongea na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO) uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa TAHLISO Bw. Stanslaus Kadugalize.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO) kutoka Chuo Kikuu cha Bugando Bw. Elia Kandonga akiongea katika mkutano kati ya TAHLISO na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na kufanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wahitimu bora wa vyuo vikuu mbalimbali wakimsikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandishi Stella Manyanya katika hafla iliyoandaliwa na Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO) ili kuwapongeza na kufanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO) kutoka vyuo mbalimbali nchini katika picha ya kumbukumbu na viongozi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) waliokutana katika Chuo Kikuu cha Mt. John mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.

Viongozi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO) wamekutana mjini Dodoma mwishoni mwa wiki ili kubadilishana mawazo na kukubaliana kuendeleza ushirikiano ili kutatua kero za wanafunzi.

Katika mkutano huo, uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu John, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TAHLISO kutoka taasisi za elimu ya juu nchini wakiongozwa na Mwenyekiti wao Bw. Peter Kadugalize walikutana kwa siku nzima na viongozi wa HESLB walioongozwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Jerry Sabi na kujadiliana njia bora za kutatua kero za wanafunzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Linaloonekana nyuma ni ndo majengo JPM anapiga nayo kelele. Tumsaidie rais wetu. Hapo hata wakitangaza siku ya kujitolea wanachuo wenyewe wanaweza kupanga rangi. Ankal tafadhali wafikishie ujumbe na uwashauri. Sio kila kitu kinahitaji wakandarasi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...