Ni kwa Mafunzo ya Uongezaji Thamani
Madini kwa Wanawake
Teresia
Mhagama, Arusha
Mkuu wa Wilaya
ya Arusha, Fadhili Nkurlu ameipongeza Kamati ya
Maandalizi ya Maonesho ya Kimataifa ya
Madini ya Vito, Arusha kwa kutoa
ufadhili wa mafunzo ya Ukataji na Ung’arishaji
wa madini ya vito kwa wanawake 29
kupitia Mfuko wa Kuwaendeleza Wanawake katika Tasnia ya Madini ya Vito.
Nkurlu alitoa pongezi hizo
wakati akifungua maonesho ya Tano
ya Kimataifa ya Madini ya Vito, yaliyoanza tarehe 19- 21
jijini Arusha na kuhudhuriwa na takriban washiriki 900 kutoka ndani na nje ya
Tanzania.
Aidha, alitumia fursa hiyo kuwataka
wadau katika sekta ya madini ya vito
kuwaajiri wanafunzi hao pindi wanapohitimu mafunzo yao na kuongeza kuwa,
desturi ya kuchangia katika kuendeleza sekta ya madini ya vito ni jambo ambalo
linahitaji kuendelezwa na wadau wote ili kuweza kuendeleza sekta hiyo.
Alisema kuwa, Serikali kupitia
Kituo cha Jemolojia Tanzania inaendelea kuboresha mafunzo hayo yanayotolewa
katika kituo hicho kwa kuanzisha kozi mpya za lapidary machine na kuongeza kuwa, kabla ya wanafunzi
18 wanaosoma sasa kituoni hapo kuhitimu, watapata mafunzo ya vitendo katika
viwanda mbalimbali vinavyoongeza thamani katika madini ya vito.
Aliongeza kuwa, Wizara ya Nishati na Madini inaendelea kukiboresha
Kituo hicho cha Jemolojia kwa kuanzisha kozi za Jemolojia, usonara na hivi sasa
iko katika hatua za mwisho za kukamilisha ununuzi wa vifaa ili viweze kutumiwa katika kozi zinayotarajiwa kuanza mwezi Septemba mwaka
huu.
Alisema kuwa, hizo ni miongoni
mwa jitihada zinazofanywa na Serikali ili
kutekeleza Sera ya Madini ya mwaka 2009 na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka
2025 ambazo kwa pamoja zinahamasihsa shughuli za uongezaji thamani madini
hapahapa nchini ili kuongeza kipato, ajira kwa watanzania na hivyo kukuza
uchumi wa nchi.
Mfuko wa kuwaendeleza wanawake
katika tasnia ya Ukataji na Ung’arishaji wa madini ya vito ulianzishwa mwaka 2012
na Kamati ya Maandalizi ya Maonesho ya Vito ambayo ilianzisha harambee ya
kuwawezesha wanawake kupata mafunzo hayo ya Uongezaji thamani madini.
Darasa la Awamu ya kwanza la
mafunzo hayo lilianza Novemba 10, 2014 ambapo wanawake wa kitanzania 15 walihitimu mafunzo husika.Vilevile Darasa la Awamu ya Pili la mafunzo ya
uongezaji thamani madini lilianza Agosti 3, 2015 ambapo wanafunzi 14 walihitimu
ambapo darasa linaloendelea kwa sasa lina wanafunzi 18.
Ufadhili wa masomo kwa
wanafunzi hao wanawake unajumuisha fedha za chakula, kujikimu, nauli, ada ya
miezi Sita, matumizi ya vifaa vinavyohitajika wakati wa mafunzo hayo na
malighafi zinazohitajika kwa ajili ya mafunzo husika.
Viongozi wa Kamati ya Maonesho
ya Vito Arusha ni Peter Pereira ambaye ni Mwenyekiti na Katibu wa Kamati ni
Elias Kayandabila ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...