Hivi juzi tumeshuhudia ufunguzi wa daraja la Kigamboni ambalo Mh. Rais Dr. John Pombe Mgufuli alilipa jina la daraja la Nyerere. Daraja hili ni matunda ya uwekezaji wenye tija unaofanywa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii la NSSF.

Shirika hilo kwa kushirikiana na serikali limeweza kujenga daraja lenye urefu wa mita 680 likiwa na barabara sita; tatu zikielekea Kigamboni na tatu zikitokea Kigamboni.  Daraja hili lina njia ya watembea kwa miguu yenye upana wa mita 2.5 kila upande.

Daraja hilo limejengwa kisasa na kampuni ya  China Railway Construction Engineering Group iliyotekeleza mradi huo kwa kushirikiana na kampuni ya China Railway Major Bridge Group kutoka nchini China.

 Kukamilika kwa ujenzi wa daraja hili, kumejumuisha barabara za kufika katika daraja hili zenye jumla ya urefu wa kilomita 2.5. Katika ujenzi wa daraja hili, Shirika la NSSF limetoa asilimia 60 ya gharama za Ujenzi na Serikali asilimia 40 ya gharama hizo.

 Akizungumza na waandishi wa habari waliotembela daraja hilo hivi karibuni, Meneja wa Mradi huo kutoka NSSF, Muhandisi Karim Mattaka alisema daraja la Kigamboni limejengwa ili kuondoa kero ya siku nyingi ya usafiri kwa wakazi wa Kigamboni na wakazi wa Dar es Salaam kwa ujumla, kuimarisha hali ya uchumi wa Mkoa huu wa Dar es Salaam, mikoa ya jirani na nchi kwa ujumla pamoja na kuimarisha hali ya uchumi wa shirika, kuliwezesha shirika kuboresha na kulipa mafao kwa kutunza thamani ya fedha kupitia kitega uchumi hiki.

Faida zitokanazo na uwekezaji huo kwa mujibu wa Muhandisi Mattaka ni faida ya moja kwa moja kwa wanachama kwani huingizwa katika akaunti zao pindi wanapochukua mafao yao pamoja na kulipia matibabu yatolewayo bure kwa wanachama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...