Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ameitaka Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA), kufanya tafiti na kuangalia fursa zitakazoiwezesha kupata mapato kutokana na kazi inazozifanya.
Amesema iwapo Mamlaka hiyo itafanya kazi kwa uadilifu na uaminifu itaongeza idadi ya watu inaowahudumia kwa mwaka nchini na hivyo kusaidia wadau mbalimbali wa sekta za Kilimo, Ujenzi, Afya, Uvuvi kufanya kazi kwa faida.
Prof. Mbarawa amekagua vitengo cha takwimu za hali ya hewa, hali ya hewa ya kilimo na Utabiri na kusisitiza kuwa ni wakati wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa teknolojia ya kisasa ili kuhudumia wadau wengi kwa wakati mmoja.
“Hakikisheni taarifa zenu zinawafikia watu wengi hususan wale wanaozihitaji taarifa hizi kwa kutekeleza shughuli zao kiuchumi”. Amesema Prof. Mbarawa.
Naye Mkurungenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi amemhakikishia Prof. Mbarawa kuwa Mamlaka hiyo inafanya utabiri  kwa usahihi wa asilimia 80 na ni miongoni mwa Mamlaka inayofanya vizuri katika huduma za utabiri barani Afrika.
“Taarifa zetu ni sahihi na kila baada ya dakika 15 tunatoa taarifa zinazoonyesha hali ya hewa nchini”. Amesema Dkt. Kijazi.
Dkt. Kijazi amesema mamlaka hiyo imejipanga kuongeza uelewa wa watumiaji wa hali ya hewa hapa nchini ili kuwezesha wadau wa hali ya hewa kunufaika kikamilifu na utabiri unaotolewa na Mamlaka hiyo.
Imetolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Mtaalam wa kusoma utabiri wa hali ya hewa Hellen Msemo akimuonyesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano namna taarifa za utabiri wa hali ya hewa zinavyorekodiwa na kutumwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisoma ramani ya utabiri wa hali ya hewa katika chumba maalum cha kusoma ramani wakati wa kukagua ofisi za Mamlaka ya hali ya hewa nchini.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Watatu kushoto) akifafanua jambo kwa wafanyakazi  wa mamlaka ya hali ya hewa nchini (Hawapo pichani) huku Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agness Kijazi ( Watatu kulia) akifuatilia kwa makini.
 Mtaalamu wa maswala ya hali ya hewa nchini Didasian Kankesha akifuatilia utabiri kabla ya uhakiki na kuutangaza kwa wadau.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa viongozi wa TMA kuhusu namna ya kufanya kazi kwa kuzingatia teknolojia ya kisasa ili kuhudumia wadau wengi kwa wakati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...