Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed alisema ni vyema kwa Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo wakajenga tabia ya kukubali kukosolewa na wafanyakazi walio chini yao zinapotokea hitilafu za kiutendaji wakati wanapotekeleza majukumu yao ya  kazi.

Mh. Aboud alisema hayo katika kikao cha kwanza alipokutana na Viongozi wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar kushika wadhifa wa kuiongoza Wizara hiyo Kikao kilichofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar. 

Alisema Wananchi walio wengi wameanza kujenga matumaini yanayotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika utendaji wa kipindi cha Pili cha Awamu ya Saba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Dr. Ali Mohammed Shein.Mh. Aboud alieleza kwamba Miaka mitano ijayo itakuwa ya kasi katika utendaji wa Serikali kuu iliyojikita zaidi kuimarisha uchumi na kusimamia Maendeleo kwa kutegemea rasilmali  na vianzio vyake vya mapato.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alielezea matumaini yake kutokana na umakini wa Viongozi walioanza kukabidhiwa majukumu ya kusimamia Taasisi za Umma katika maeneo mbali mbali.
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa kwanza kutoka kulia akiwa katika kikao cha kwanza na Viongozi wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein kuiongoza Wizara hiyo.
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim akielezea faraja kwa niaba ya watendaji wa ofisi hiyo wakati viongozi wa Taasisi za Ofisi hiyo walipokutana kwa mara ya kwanza na Waziri wao Mh. Mohammed Aboud Mohammed ofisini vuga Mjini Zanzibar.
Waziri Aboud akiwaagiza wasaidizi wake kuwasimamia vyema watendaji wao katia kutekeleza majukumu yao yanayotarajiwa kuongezeka kutokana na kazi ya utendaji wa Serikali wa kipindi cha Pili cha Awamu ya Saba.Picha na – OMPR – ZNZ.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...