Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed alisema ni vyema kwa Viongozi wa Taasisi
zilizo chini ya Ofisi hiyo wakajenga tabia ya kukubali kukosolewa na
wafanyakazi walio chini yao zinapotokea hitilafu za kiutendaji wakati wanapotekeleza
majukumu yao ya kazi.
Mh. Aboud alisema hayo katika kikao cha kwanza alipokutana
na Viongozi wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Ofisi hiyo mara baada ya
kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar kushika wadhifa wa kuiongoza Wizara hiyo
Kikao kilichofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Alisema Wananchi walio wengi wameanza kujenga
matumaini yanayotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika utendaji wa kipindi
cha Pili cha Awamu ya Saba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na
Dr. Ali Mohammed Shein.Mh. Aboud alieleza kwamba Miaka mitano ijayo itakuwa
ya kasi katika utendaji wa Serikali kuu iliyojikita zaidi kuimarisha uchumi na
kusimamia Maendeleo kwa kutegemea rasilmali
na vianzio vyake vya mapato.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar alielezea matumaini yake kutokana na umakini wa Viongozi walioanza
kukabidhiwa majukumu ya kusimamia Taasisi za Umma katika maeneo mbali mbali.
Waziri Aboud akiwaagiza wasaidizi
wake kuwasimamia vyema watendaji wao katia kutekeleza majukumu yao
yanayotarajiwa kuongezeka kutokana na kazi ya utendaji wa Serikali wa kipindi
cha Pili cha Awamu ya Saba.Picha na – OMPR – ZNZ.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar wa kwanza kutoka kulia akiwa katika kikao cha kwanza
na Viongozi wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Ofisi hiyo mara baada ya
kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein kuiongoza Wizara
hiyo.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim akielezea faraja kwa niaba ya
watendaji wa ofisi hiyo wakati viongozi wa Taasisi za Ofisi hiyo walipokutana
kwa mara ya kwanza na Waziri wao Mh. Mohammed Aboud Mohammed ofisini vuga Mjini
Zanzibar.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...