Waandishi wa habari wameaswa kujiendeleza kielimu katika fani ya uandishi wa habari na taaluma nyingine ili waweze kukabiliana na kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.
 
Wito huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mhadhiri Chuo Kikuu Huria Dr. Hamza Kondo alipokuwa akizindua kitabu chake kiitwacho Watchdog Journalism in Tanzania a Sustainable Struggle ambapo kwa Kiswahili ni “Uandishi Habari Huru Tanzania ni mapambano endelevu”.
 
Dr Kondo amesema lengo la kitabu hicho ni kuwaelimisha na kuwaasa waandishi wa habari na wataaluma ya habari kuzidi kuithamini taaluma hiyo licha ya changamoto zinazowakabili.Amesema kitabu hicho kinazungumzia uhalisia wa uhuru wa habari nchini, hivyo kinafaa kufundishia taaluma ya habari katika vyuo vikuu na vyuo vya kati nchini.
 
Aidha, Mhadhiri huyo ameongeza kuwa ili fani ya taaluma ya habari iheshimike ni lazima iwe na bodi ya wataalamu waliobobea ambayo itaundwa na wasomi wa taaluma husika ili kusimamia maadili ya taaluma hiyo na kuchukua hatua kwa wanataaluma watakaokiuka maadili.
 
Mbali na hayo Dr Kondo ametoa zawadi ya vitabu kwa baadhi ya vyombo vya habari nchini likiwemo gazeti la Jamuhuri, gazeti la majira, gazeti la Habari Leo, gazeti la Mwananchi na gazeti la Nipashe.
 
Na Beatrice Lyimo - MAELEZO

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...