
MAKAMO mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Zanziba Dkt.Ali
Mohamed Shein (Pichani)amewapongeza wanachama na viongozi katika wilaya ya
Micheweni kwa kukiamini na kukiweka madarakani chama hicho katika
Uchaguzi Mkuu wa Marudio mwaka huu.
Dkt.Shein alisema kwamba ushindi uliopatikana katika uchaguzi huo
umetokana na nguvu na nia za dhati za wananchi waliamua kwa pamoja
kuichagua CCM kwa kura nyingi ili iendelee kuongoza dola.
Akizungumza na mamia ya wafuasi wa CCM wakiwemo Mabalozi,wenyeviti na
Makatibu wa matawi na maskani za Wilaya ya Micheweni Kichamanhuko
katika ukumbi wa Chuo cha Kiislamu Pemba, alisema baada ya kumalizika
kwa uchaguzi mkuu wa marudio kwa sasa CCM inaendelea na utekelezaji wa
Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 ili wananchi wapate
maendeleo endelevu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...