Na  Bashir  Yakub.
Mara  kadhaa  imetokea  mtu  anahitaji  kununua  ardhi  sehemu  ambayo yeye  haishi.  Mara  nyingi  hii  imetokea  kwa  walio  nje  ya  nchi.  Mtu  anaona  kiwanja  au  nyumba  kwenye  mtandao  au  kwenye  chombo  chochote  cha  habari  lakini  anakosa  namna  ya  kununua. 

 Saa  nyingine  hufanya  mawasiliano  na  wahusika  hadi  kufika  bei lakini  tatizo  likawa  ni  vipi  atanunua.  Vipi  ataweza  kununua bila  kuhitaji kurudi  nchini hubaki  mtihani.

Anapiga  mahesabu  ya  nauli  kwenda  na  kurudi, usumbufu, ratiba  ya  kazi  zake  na  mambo  mengi   anaona haiwezekani.  Anashindwa  kununua   kwasababu  tu  ya  umbali.  Na  hii  si  kwa  walio  nje  ya  nchi  tu  bali  hata walio  mikoa  tofauti   pia  hili  huwatokea  japo  si  sana. 

Pia   wako  wengine  ambao  tatizo  sio  kuwa  mbali  na  maeneo  wanayotaka  kununua  bali  wana shughuli  nyingi  mno  kiasi  cha  kutopata  mda  mzuri   wa  kufuatilia  miamala  ya  manunuzi  mpaka  mwisho. 

Hawa  wote  na  wengine   wengi  kupitia  makala  haya watajua  namna  ambavyo  wanaweza  kununua ardhi  bila   kuhitajika  kuwepo. 

1.TARATIBU  ZA  KUNUNUA  ARDHI.
Imewahi  kuelezwa  mara  nyingi  namna  bora  na  salama  ya  kununua  ardhi lengo  likiwa   hasa  kuepuka  utapeli, kuepuka kuuziwa  mara  mbili  au  zaidi  kwa watu tofauti( double  allocation), kuepuka  kununua  maeneo  yenye  migogoro  mahakamani,  maeneo  yaliyowekewa  mazuio( injuction & caveat), kuepuka  kununua  maeneo  yasiyo  na  hati  za  mirathi,  yaliyowekwa  dhamana n.k. 

Tulieleza  hatua  za  kufuata  ili  kuyaepuka  haya sambamba  na  maandalizi   ya  mkataba  wa  mauzo  yanayokidhi   vigezo  mahususi   vya  kisheria.  Ni vema  kila mda kusisitiza  kuwa migogoro  ya  ardhi  inazidi  kuongezeka  kila  siku  na  watu  hupata  hasara  kila  kukicha. Lakini  unaweza  kuepuka    kuwa  sehemu  ya  migogoro  hii  ikiwa  tu  utafuata  taratibu  pamoja  na  kuzingatia  maandalizi  mazuri   ya  mkataba  wa  mauzo unaokidhi  vigezo  vya  kisheria.
KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 03, 2016

    Ila sitofanya hivyo kwani atanikata pesa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...