Mhe. Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania 2016/17 mara baada kumalizika kwa kikao  baina yao kilichofanyika   mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Mikutano wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) mjini Dodoma. 
Mhe. Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Miss Tanzania, Lilian Kamazima  mara baada ya kumalizika kwa kikao cha baadhi ya wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania 2016/17 kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa TBC mjini Dodoma. Kikao hicho kilijadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuiomba Serikali iwasaidie kupata wadhamini wa mashindano hayo kitaifa yanayotarajiwa kufanyika mwezi wa kumi mwaka huu.
Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania 2016/17 wakimsikiliza Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura wakati wa kikao  baina yao kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Mikutano wa Shirika la  Utangazaji la Taifa (TBC) mjini Dodoma.
Picha na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...