
Naibu waziri wa maliasili na utalii Mh. Ramo Makani, Amesema serilikali ya awamu ya tano itahakikisha jamii zinazo ishi karibu na shamba la taifa la sao hill, lenye tarafa maalum (4) za Mgololo, Ihalimba, Ihefu na Irundi zinakuwa za kwanza kunufaika na mgao wa vibali vya uvunaji wa misitu ili zishiriki kikamilifu katika kulinda, kuhifadhi na kuiboresha misitu hiyo kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Taarifa ya kitengo cha habari na mawasiliano cha halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, imebainisha kuwa naibu waziri Makani ameyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi katika shamba la miti la Taifa la sao hill wilayani Mufindi Mkoani Iringa.
Amesema, ili wananchi waone kuwa msitu huo ni mali yao kama Watanzania, ni lazima wawe wa kwanza kufikiriwa wakati wa ngao wa vibali vya uvunaji kupitia jumuia watakazo ziunda katika maeneo yao.
Akizungumzia suala la utoaji wa vibali vya uvunaji wa misitu amesema, msitu waSao Hill na mingine nchini ni mali ya Taifa, hivyo, ni haki kwa Mtanzania yeyote popote nchini kupata kibali na akasisitiza kuwa kwa mwaka huu huwenda vibali vikachelewa kutoka kwa kuwa wizara yake iyapiti maombi kwa umakini ili kupunguza malalamiko ya upendeleo katika utoaji vibali.
shamba la Miti la Sao hill lililopo Wilayani Mufindi ni la kwanza kwa ukubwa nchini kati ya mashamba 18 ya Taifa, ilikiwa na hekita zaidi ya laki moja na 35 elfu na lilianzishwa rasmi mwaka 1960.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...