Na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma.

SERIKALI imepiga marufuku upakiaji wa mizigo kupita kiasi (lumbesa) katika magunia kuanzia mwaka ujao wa fedha.

Kauli hiyo imetolewa jana Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb) wakati akijibu hoja mbalimbali za Wabunge wakiochangia hotuba ya Wizara yake.

Amesema kuwa, kuanzia mwaka ujao wa fedha, Vyombo vy Dola vitakamata wafanyabiashara wote watakaokuwa wanapakia lumbesa.

Mhe. Mwijage alisema kuwam upakiaji huo wa mizigi kupita kiasi unawasababishia wizi kwa wakulima ambapo ametoa wito kwa wakulima na wafanyabiashara nchini kutumia vipimo halali wakati wanaponunua na kuuza mazao yao mbalimbali.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo ametoa wito kwa wakulima kuacha tabia ya kuuza mazao yao yakiwa shambani au kabla ya kukomaa.

Alisema kuwa hali hiyo inawarudisha nyuma na kuwapunja wakati wangesubiri mazao yakomae wangepata fedha za kutosha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 10, 2016

    kwani lumbesa ndo inazidisha mzigo? kama serikali nyie ilitakiwe mpime pale mizani tu na msihangaike na staili za ufungaji mizigo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...