Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafirishaji Nchi Kavu na Majini, Johansen  Kahatano akizungumza na waahabari juu ya nauli za mabasi yaendayo kasi haraka katikati ya jiji la Dar es Salaam,kutoka  Mbezi mwisho –Kimara –Kivukoni nauli ni800 mwanafunzi 200. Mbezi mwisho –Kimara –Kariakoo nauli 800,mwanafunzi200. Morocco-Kimara –Mbezi Mwisho nauli 800,mwanafunzi 200. na Morocco-Kivukoni nauli 650. mwanafunzi 200. Kariakoo – Morocco nauli 650.mwanafunzi 200.viwango vipya vya nauli vinapaswa kuanza kutumika rasmi Mei,12 mwaka huu, mkutano huo umefafanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Traffic  wa Kanda, Magembe Seni.
Sehemu ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafirishaji Nchi Kavu na Majini, Johansen  Kahatano leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu, ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 09, 2016

    Je kuna uwezekano wa wasafiri wa mabasi hayo ya kasi kununua ''tiketi'' ya msimu kwa kulipa ''in-advace'' kwa mwezi mzima akapanda mabasi hayo ya route zote kwa mwezi mzima kwa kuonesha kadi ya malipo aliyolipia yaa mwezi mzima in-advance na hivyo kupunguza kulipia kila siku kwa kila route.

    Utaratibu wa kulipia tiketi in advance kama wa voucher za simu/umeme pia kuwezesha kampuni ya mabasi ya mwendo kasi kupata malipo in-advance kununulia mafuta, vipuri pia kuingia maktaba na makapuni ya mafuta/matairi/vipuri/ununuzi au ku-''hire'' mabasi ya ziada kwa pesa hizo za ''advance''

    Nakumbuka kampuni ya Usafirishaji ya Dsm a.k.a UDA Enzi za Mwl. Nyerere walikuwa na utaratibu huo wa kulipa ina Advance na pia nikaukuta nchi nyingi za ulaya wanafanya utaratibu huo na ukiwepo usimamizi mzuri basi hakuna shaka route za mabasi ya mwendo kasi DSM utapanuka mpaka Wazo Hill, Mbagala n.k

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 10, 2016

    Ndivyo inavyotakiwa iwe. Shida tunataka vitu vya gharama lakini uwezo wa kuvihudumia ni mdogo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...