Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe akifungua warsha ya siku mbili kwa Wadau wa Mradi wa kusindika gesi asilia nchini (LNG) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Utafiti (TPDC), Bw. Kelvin Komba akielezea mbele ya waandishi wa habari lengo la warsha ya siku mbili kwa Wadau wa Mradi wa kusindika gesi asilia nchini (LNG) jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Mradi wa kusindika gesi asilia nchini (LNG) wakifuatilia warsha hiyo.

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linaendesha warsha ya siku mbili ya Wadau wa Mradi wa kusindika gesi asilia kuwa kimiminika nchi (LNG). Akifungua Warsha hiyo kwa Niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe alisema warsha hiyo inalenga kuwakutanisha wadau wanaoshiriki katika utekelezaji wa Mradi huo.

Aliongeza kuwa warsha hiyo pia imekusudia kutengeneza mazingira shirikishi kwa wadau hao kabla ya kuanza kutekeleza ujenzi wa wa Mradi huo. Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika gesi asilia kwa matumizi ya ndani na kusafirisha nje ya nchi unatarajiwa kujengwa eneo la Likong’o katika Manispaa ya Lindi.

Warsha hiyo inawakutanisha wadau kutoka Wizara ya Nishati na Madini, TPDC, Taasisi kutoka Serikalini na Makapuni ya Wawekezaji ya Mafuta na Gesi Nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...