Yale mabasi yaendayo haraka, tuliyokuwa tukiyasubiri kwa hamu kwa kipindi kirefu, hatimae leo yameanza kazi rasmi kwa ruti zote zilizopangiwa. pamoja na kuanza kwa kazi, lakini bado wanachangamoto ya matumizi ya njia yake, kwani bado kuna baadhi ya vyombo vya usafiri vimekuwa vikiitumia njia yake hiyo kana kwamba ni jambo la kawaida tu. Leo Kamera ya Mtaa kwa Mtaa imezungukia eneo la Kariakoo na kujioneka hali halisi katika barabara hiyo na kukuletea wewe mdau ujionee mwenyewe na kutoa maoni yako ya nini kifanyike ili jambo hili likae kwenye mstari ulionyooka. Picha na Emmanuel Massaka.
Daladala hili likiwa limeifunga kabisa njia hiyo kwa lengo la kukatisha barabara hiyo kurudi lilikotoka baada ya kuona chombo chenye njia yake kikichomoza mbele yake.
Bodaboda na Watembea kwa miguu wakijidai katika barabara hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 10, 2016

    Ssa hawa watembea kwa miguu kwa nini wanatembea katika kati ya barabara, na Bodabodaje?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 10, 2016

    Lazima ifikia mahali watanzania waache ujinga na ukorofi kwa kigezo cha ugumu wa maisha. Ndio maana Rais anakuwa mkali watu wanaanza oh sijui nini. Hawa wote ilibidi wachukuliwe sheria. Lazima watu wafuate sheria.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 10, 2016

    Inabidi ziwekwe kamera hapo watakao pigwa picha walipe fine kubwa na dereva kunyang'anywa leseni ....au serikali iweke fence

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...