KUHUSU MASHOTO
Kwa miaka mingi, jamii nyingi zimekuwa na mila potofu kuhusiana na mashoto. Wengi wamekuwa wakiita mkono wa kushoto kama mkono wa shetani. Jamii nyingi zimekuwa na kawaida ya kulazimisha kuwabadili watoto wao mkono wa kutumia pindi wagunduapo watoto hao ni mashoto. Jamii hizo zimekuwa zikiamini kuwa mashoto ni ulemavu ama mkosi. 

Kwanza Kabisa nianze na kutoa ufafanuzi wa maneno haya kwa Kiswahili yaani mkono wa kushoto na mkono wa KULIA ni utohozi tu kutoka kwa lugha na tamaduni nyingine na utakuta kimantiki hayashabihiani kabisa linapokuja suala la tasfiri kwenda kwenye lugha yetu maarufu ya kiingereza ambayo ni ya pili kwa matumizi nchini.

Nashawishika Kuamini kwamba huenda matumizi ya neno mkono wa kulia unatokana na urithi wa utamaduni wa kutumia mkono huo kwa KULIA CHAKULA na ndio maana wengi wameathirika kisaikolojia tu kwa kuona mtoto anatumia mkono wa kushoto kwa KULA ilihali mkono huo una maarufu wake hasa kwenye maeneo Fulani NYETI ya haja kubwa na ndogo wengi huuita mkono wa kushoto kama ‘kono la mavi’.  Katika Kilatini, mkono wa kushoto umekuwa ukitwa ‘sinitra’ ambayo humaanisha kitu kiovu. 

Kwa Bahati mbaya sana katika makuzi ya hasa kiafrika, utamaduni wa kutumia mkono wa kushoto haujazoeleka sana na ikitokea mtoto amezaliwa mashoto itafanyika kila jitihada kumbadilisha azoee kutumia mkono wa KULIA jambo ambalo si tu kwamba ni ukatili bali pia linadhoofisha na kudumaza maendeleo ya mtoto ……Nikikuuliza swali wewe unayetumia mkono wa kulia itumike nguvu ya kukubadilisha utumie mkono wa kushoto unadhani ni rahisi?

Naamini kabisa kwamba wengi miongoni mwetu tumepitia kadhia hii aidha kwa kutenda ama kutendewa ama vyote

Nikupe habari njema kifupi tu kwamba kama umezaa mashoto basi una miongoni mwa watu wenye Intelligent Quotient (IQ) kali sana duniani

Mpe nafasi ya kuwa independent wakati unamkuza, mwache achague mwenyewe lolote lile, halafu we ndio umrekebishe kama kachagua baya na uwe tayari kumpa maelezo maana wanadadisi kweli... baaada ya kupita kipindi cha utoto (After his/her early teens) utagundua nilichokuambia kuwa ni genious.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...