Uendeshaji wa magari wa aina hii unaleta kero na adha kubwa kwa madereva wengine barabarani,Uendeshaji huu wa kutofuata sheria za usalama barabarani,Jeshi la Polisi liongeze kasi kupambana na kuwadhibiti vilivyo madereva wa aina hii,ambao kwa makusudi mazima huamua kukiuka sheria hizo na kupelekea usumbufu mkubwa kwa madereva wengine wenye kutii sheria.
Kamanda wa Polisi, Kikosi cha usalama barabarani Mohammed Mpinga ameeleza leo kuwa ongezeko la makosa ya watumiaji wa barabara
limechangia jeshi hilo kuagiza askari wake kukamata watumiaji kumi kila
siku wanaovunja sheria za barabarani.
Kamanda Mpinga alibainisha Makosa
yanayofanywa na madereva wengi ni pamoja na kuyapita magari mengine
bila kuchukua tahadhari (Overtaking),(tazama picha juu na chini), kupita taa nyekundu, kuendesha kwa
mwendo kasi, kuendesha wakiwa wamelewa, madereva bodaboda kutovaa kofia
ngumu, kubeba mishikaki, kutokuwa na leseni na pikipiki kutokuwa na
Bima.
Na sisi Globu ya Jamii katika kuliunga mkono Jeshi la Polisi,Kikosi cha usalama barabarani,liendelee kukaza uzi kukamata makosa kumi kila siku ya madereva wazembe barabarani mpaka tunyooke.
Hili jambo Jeshi la polisi limeshindwa kusimamia kwa juhudi thabiti uendeshaji mbovu. Madereva wanapata (wanajenga) kiburi kwa vile sharia imelifumbia macho hili jambo. Wazee wa favor mmepewa target ya magari kumi kwa siku.. Kazi kwenu...
ReplyDelete