
Kwenye ratiba hiyo, City imepaga kucheza michezo mitatu ugenini, ambapo itaanza kwa kushuka ‘dimbani’ Kamuzu Stadium jijini Blantyre Juni 18 kucheza na vigogo wa soka nchini Malawi, Big Bullets ambapo kwa mujibu wa waandaaji, mchezo unatarajia kushuhudiwa na watazamaji wengi hasa ukizingatia ushawishi wa timu hiyo kwenye soka la nchi hiyo.
Mkuu kitengo cha habari na mawasiliano kwenye kikosi cha City, Dismas amesema kuwa mchezo wa pili nchini humo utachezwa jijini Lilongwe na utakuwa dhidi ya wenyeji Civo United, kwenye dimba la Civo Stadium hii itakuwa ni Juni 21 na kumalizia na Mzuni Juni 25.
“Baada ya mchezo huo wa pili jijini Lilongwe,tutarudi kwenye mji ulio kaskazini mwa nchi hiyo, Mzuzu, hapo tutacheza na wenyeji wetu Mzuni Fc, Juni 25 huu utakuwa mchezo wa mwisho kwenye ziara hii ya michezo ya kirafiki, baada ya hapo tutarudi nyumba tayari kwa michezo mingine ambayo imepangwa ukiwemo dhidi ya Simba tutakaocheza Morogoro,"amesema Ten.
Kama mambo yatakwenda sawa, ratiba hii inaweza kuwa na ongezeko la michezo miwili ya kirafiki katikati ya mwezi julai kabla ya mchezo wa mwisho wa mwezi huo dhidi ya Simba na mwingine mwanzoni mwa mwezi wa nane kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...