Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii.

Mkongwe wa Soka nchini Nigeria ambaye aliwahi kuwa Nahodha wa Kikosi hicho cha Super Eagles na kuwahi kunyakua taji la AFCON akiwa kama Kocha na Mchezaji, Steven Keshi amefariki Dunia ghafla.

Kifo cha Keshi imeelezwa kuwa alikua akisumbuliwa na matatizo ya Moyo kwa muda mrefu.

Keshi aliwahi kunyakua taji la AFCON mwaka 1994 kabla ya kutupwa nje ya Michuano ya Kombe la Dunia katika hatua ya Robo Fainali mwaka huohuo wa 1994.

Ameinoa Super Eagles katika kipindi cha awamu tatu,akiiongoza kunyakua taji la AFCON mwaka 2013 nchini Afrika ya Kusini na kuifikisha timu hiyo hatua ya 16 Bora katika Michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014.

Keshi hakusaini mkataba wa kuinoa Nigeria baada ya kumalizika Michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil licha ya timu hiyo kushindwa kufuzu AFCON mwaka 2015.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...