Mkuu wa wilaya ya Temeke Sophia Mjema kwa kushirikiana na Taasisi ya GSM Foundation wamekabidhi mifuko 600 ya saruji kwa Shule ya Msingi Mbande iliyopo kata ya Chamazi ikiwa ni jitihada za kuboresha elimu kwa kukabiliana na changamoto za Uwepo wa madarasa uliokuwa unaikabiri shule hiyo kwa muda mrefu.

Licha ya kukabidhi mifuko hiyo 600 ya Saruji Mkuu wa wilaya Mjema ameahidi kufanya jitihada za kutafuta madawati 400 kukabiliana na changamoto za wanafunzi. kukaa chini huku akiongeza kuwa atalishughulikia ipasavyo suala là Uhaba wa walimu kwa shule hiyo kwa kuongeza walimu 40.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Dauden Mwakyambiku amesema msaada huo unatija kwao kwani tangu kuanza kwa sera ya elimu bure kumekuwa na changamoto ya ongezeko la wanafunzi ambalo linahitaji madarasa, ambapo shule hiyo inawanafunzi 5,815 huku vyumba vya madarasa vikiwa 16 na serikali imeagiza kila chumba kukaa wanafunzi 45.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (wanne kulia) na Meneja Mkuu wa GSM Foundation Shannon Kiwamba (katikati) pamoja na wadau wengine, wakikabidhi mifuko hiyo 600 ya Saruji kwa uongozi wa Shule ya Msingi Mbande leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa wilaya ya Temeke Sophia Mjema akiwa pamoja na uongozi wa Taasisi ya GSM Foundation wakiwa kwenye stoo ilipohifadhiwa saruji hiyo.
Sehemu ya wazazi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Temeke Sophia Mjema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...