Mwenyekiti mpya wa Bodi ya NHIF, Mama Anne Makinda (kushoto) akiwasili kwenye Makao Makuu ya NHIF kwa siku ya kwanza mara baada ya kuteuliwa na kuwa mwenyekiti wa bodi wa mfuko huo leo jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NHIF, Raphael Mwamoto pamoja na Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), Eugen Mikongoti. Mh. Makinda alipata, pia fursa ya kuwa na mazungumzo mafupi na uongozi wa Mfuko huo chini ya Kaimu Mkuu wake, Bernard Konga na vilevile alitembelea baadhi ya ofisi ikiwemo kituo cha utunzaji nyaraka za mfuko kwa njia za kielektroniki, kituo cha huduma kwa wateja na kituo cha utunzaji taarifa za Mfuko kwa lengo la kuona jinsi zinavyofanya kazi leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mama Anne Makinda akiwa katika chumba maalum cha kuhifadhi nyaraka mbalimbali za wanachama wa mfuko huo leo mara baada ya kufanya ziara kutembelea Makao Makuu ya Mfuko huo leo jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti mpya wa Bodi ya NHIF, Mama Anne Makinda akionyeshwa sehemu ya kuhifadhia kumbukumbu za wanachama mara baada ya kufanya ziara kutembelea Makao Makuu ya Mfuko huo leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti mpya wa Bodi ya NHIF, Mama Anne Makinda akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...