Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues amewakumbusha wadau wa urithi wa dunia na maeneo ya hifadhi kufanyakazi kwa pamoja kwa lengo la kuhifadhi na kuyaendeleza maeneo hayo bila kuondoa ushiriki wa wananchi wanayozunguka.
Kauli hiyo ameitoa katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia mjini Marangu Moshi, kufuatia makubaliano na serikali ya Tanzania.
Alisema akizungumza na washiriki kwamba UNESCO inachofanya ni kuanzisha safari ambayo inaweza kuwa ngumu na ndefu lakini washiriki wake ni lazima kutambua namna ya kuendelea kufanya menejimenti ya maeneo ya hifadhi na urithi wa dunia kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Akifungua mafunzo hayo ambayo wataalamu ni washiriki wenyewe wakitumia njia ya kuelewa ya methodolojia ya uchambuzi wa vikwazo (Bottleneck Analysis Methodology) alisema safari ya kufanikisha menejimenti ya maeneo hayo duniani na hasa hapa nchini ni yenye changamoto nyingi na kwamba wadau wote wanatakiwa kuwa pamoja kuvishinda vikwazo hivyo na kuifanikisha safari.
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza katika warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.(Picha zote na Zainul Mzige)
Akizungumza katika warsha hiyo ambayo imechukua wadau mbalimbali wa masuala ya urithi na menejimenti zake kutoka serikalini, taasisi zisizo za kiserikali na wananchi wengine, alisema kwamba maeneo hayo yamezungukwa na wananchi na pamoja na kuwawekea sheria za kutoharibu na kuyachakaza ipo haja ya kushirikiana nao namna ya kupanga kuyaendeleza maeneo hayo huku yakiwa yamebaki katika hali inayotakiwa.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kupanga maendeleo katika maeneo ambayo ni ya urithi wa dunia, binadamu na maeneo ambayo uhai unaweza kuwepo.
Ofisa anayeshughulikia watu na maeneo yenye uhakika wa uhai: Biashara zinazozingatia mazingira na uchumi unaombatana nao kutoka Sekta ya Sayansi Ofisi ya Unesco, Dar es salaam, Myoung Su Ko akiwasilisha mada kwa washiriki wa warsha hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Resort mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
Aidha akifafanua zaidi mtawala huyo wa UNESCO nchini Tanzania amesema mafunzo hayo yamelenga kuwapa wahusika nadharia zinazofaa katika safari ndefu ambayo UNESCO nayo itashiriki na isingelipenda kumwacha hata mtu mmoja nyuma.
Mafunzo hayo yanatolewa kufuatia mpango wa UNESCO wa kutaka kuwa na uhakika na kuhami maeneo hayo ya urithi; huku mamlaka zikitoa ushirikiano ili kuwezesha malengo ya maendeleo endelevu, ambayo ndiyo ajenda ya dunia kuelekea 2030, yanafikiwa bila kuathiri maeneo tajwa.
Sehemu ya wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia waliohudhuria warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na UNESCO, mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...