Mama Maria Tereza akisisitiza jambo wakati akitoa shukrani zake kwa wanawake wa Tanzania wanaofanya miradi mbalimbali ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

MAKAMU wa Rais mstaafu wa Hispania, Maria Tereza Fernandes de la Vega Sanz (67), amesema kwamba amefurahishwa mno na mafanikio ya wanawake 15 wa Tanzania katika kipindi kifupi baada ya mafunzo waliyoyapata jijini Madrid mapema mwaka huu.

Akizungumza wakati wa chakula cha usiku alichowaandalia akinamama hao wanaotekeleza mradi wa Green Voices katika Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam usiku huu mara baada ya kutua kutoka Hispania, Mhe. Maria Tereza amesema amefarijika kuona wazo lake lililoibuka mwishoni mwa mwaka 2015 la kuwawezesha wanawake kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi limeweza kuzaa matunda.

Mama Maria Tereza ndiye anayefadhili miradi hiyo kupitia taasisi yake ya Women for Africa Foundation.
 Mama Maria Tereza Fernandes de la Vega Sanz (kushoto) akimkabidhi zawadi Balozi Getrude Mongella katika hafla hiyo.

“Ni mwaka jana tu mwishoni nilipowaza namna ya kuwawezesha wanawake, hasa wa Tanzania, katika vita ya dunia ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, lakini nafarijika kusikia kwamba wanawake wachache ambao tuliwapatia mafunzo nchini Hispania leo hii wameweza kufanikiwa kuliko hata tulivyotarajia, ni muda mfupi na mafanikio ni makubwa,” alisema.

Mama Maria Tereza alikuwa makamu wa rais wa Hispania kati ya Aprili 18, 2004 hadi Oktoba 20, 2010, na ndiye alikuwa msemaji wa serikali ya Waziri Mkuu Jose Luis Rodriguez Zapatero. Yeye ni mwanamke wa kwanza kushika nafasi hiyo katika historia ya Hispania.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...