Ghala moja lililokuwa linatumika kwa kuhifadhia mataili pamoja na vifaa vyenginevyo vya magari lililopo Sinza Lego ambalo mmiriki wake hakufahamika kwa mara moja limeteketea kwa moto jioni ya leo, chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni mataili chakavu yaliyokuwa yakichomwa moto. Pia katika eneo hilo kuna Gereji ambayo haikuathirika na moto huo mkubwa, mpaka tunaingia mitamboni, kikosi cha kuzima moto na uokoaji kilikuwa eneo la tukio kuendelea kusaidiana na wananchi kuhakikisha moto huo unazimika. Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi.
Mmoja wa kijana ambaye alifika kushuhudia tukio hilo akipanda juu ya Ghorofa baada ya kunusurika kudondokea katika moto huo.
Ghala likiwa linateketea kwa moto jioni hii Sinza Lego
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...