·         Tamasha hilo litafanyika siku ya Jumamosi, Agosti 13, 2016 katika viwanja vya posta Kijitonyama.

·         Wasanii wakubwa nchini kulishambulia jukwaa, wakiwemo Ali Kiba, Lady Jaydee, Yamoto Band, Madee, Juma Nature, Snura, Stamina, Eskide (msanii wa muziki wa singeli) na bila ya kusahau wakali wa bongo movie pia watakuwepo.

·         Watanzania wataweza kujionea jukwaani vipindi mbalimbali vinavyorushwa kupitia chaneli hiyo inayoonekana hapa nchini Tanzania na Kenya.

Wasanii wa muziki wa Bongo Flava Ali Kiba na Lady Jaydee wanatarajiwa kutumbuiza katika tamasha la kusherehekea miaka miwili tangu kuanzishwa kwa chaneli ya StarTimes Kiswahili siku ya Jumamosi ya Agosti 13, 2016 katika viwanja vya Posta, Kijitonyama.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo Mkurugenzi Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li amesema kuwa tamasha hilo linadhamiria kusherehekea kwa pamoja na wateja wao mafanikio yaliyofikiwa na chaneli ya StarTimes Kiswahili katika kuonyesha vipindi vyenye maudhui ya Kiswahili nchini Tanzania na Kenya.

“Chaneli hii mwaka huu mwezi wa Agosti inatimiza miaka miwili tangu kuanzishwa kwake mnamo Agosti mosi mwaka 2014. Chaneli ya StarTimes Kiswahili inaonekana katika nchi mbili za Tanzania na Kenya na hivyo kutoa wigo mpana kwa wasanii na watayarishaji wa vipindi hapa nchini kupata fursa ya kuonekana maeneo hayo. Vipindi vingi katika chaneli hii huangazia masuala ya filamu, muziki, burudani, vyakula, mitindo ya maisha na mavazi pamoja na tamaduni za watu wa Afrika ya Mashariki hususani kwa nchi hizo mbili ambavyo huwasilishwa kwa lugha ya Kiswahili.” Alisema Bw. Li

“Tamasha hili litahusisha shughuli mbalimbali hususani kuangazia maudhui yanayopatikana kwenye chaneli ya StarTimes Kiswahili lakini pia litapambwa na burudani kadhaa kutoka kwa wasanii watakaoalikwa. Siku hiyo watanzania watawashuhudia wasanii wakubwa wa muziki wa bongo flava jukwaani kama vile Ali Kiba, Lady Jaydee, Juma Nature, Madee, Yamoto Band, Snura na Stamina.  

Msanii wa muziki wa bongo flava Ali Kiba (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Wakimsikiliza kwa makini kulia ni Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li na kushoto ni Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian. Huawei ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL.
Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Huawei, Bw. Zhang Heng, ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la StarTimes Kiswahili linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL, Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li, Msanii wa muziki wa bongo flava Ali Kiba na Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian wakikata keki kuashiria uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. 
Waandaaji,Wadhamini na wasanii mbalimbali watakaotumbuiza kwenye tamasha la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL wakiwa katika picha ya pamoja.

Mmoja wa Wasanii atakaetumbuiza kwenye tamasha la  SEREBUKA MUSIC FESTIVAL Ali Kiba akipeana mkono na 
Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Baraza la Kiswahili jitahidini kutoka na kukemea watu wanao potosha Kiswahili hasa kwenye matangazo ya kitaifa na kimataifa, mfano hilo neno "SEREBUKA" HILI SIO NENO LA KISWAHILI na kama walitaka kusema SELEBUKA basi lingeandikwa kifasaha kama walivyoweza kumalizia sentensi nzima kwa maneno ya kingereza kwa ufasaha, tukiachia haya yaendelee bila kuwa na mlinzi wa kuitunza lugha hii basi itafika pabaya, siku hizi unaona hata magazeti yanashindwa kuandika Kiswahili fasaha hii ni aibu kwenu nyie baraza la Kiswahili kwa kukaa kimya bila kukemea hii tabia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...