Mwanafunzi bora wa somo la bailojia kitaifa kwa mwaka 2016, Bi. Anab Faisal Issa (katikati) akiwa katika picha na wazazi wake, Bw. Faisal Issa (wa pili kulia) na Bi. Beng’i Issa (wa pili kushoto) pamoja na walimu wa shule ya sekondari Feza mara baada ya kupokea tuzo katika hafla fupi iliyoandaliwa na Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa serikali kwa lengo la kuwatambua na kuwapa moyo wanafunzi kupenda masomo ya sayansi. Hafla hiyo ilifanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Afisa tawala wa wizara ya afya Bw Michael John akikabidhi cheti kwa mwanafunzi bora wa somo la bailojia kitaifa kwa mwaka 2016 kutoka shule ya Feza Bi.Anab Faisal Issa katika hafla iliyoandaliwa na Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa serikali kwa lengo la kuwatambua na kuwapa moyo wanafunzi wengine kupenda masomo ya sayansi.
Hongera Sana Miss Anab. Keep it up. Kichwa hicho ni cha wazazi wako Ambao pia ni waalimu. Hongera pia walimu wako #Feza.Dr Mwita, Jaffar, nimefurahi saana
ReplyDelete