SIMU.TV: Serikali inakusudia kuwepo kwa mpango wa uagizaji wa pamoja wa mbolea kama ilivyo mafuta ili kuweza kupanga bei elekezi. https://youtu.be/tvJ-CB08REk
SIMU.TV: Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC kimeiomba serikali kufuta adhabu ya kifo kutokana na adhabu hiyo kuenda kinyume na haki za binadamu.https://youtu.be/M9Y0LB05Vo0
SIMU.TV: Naibu waziri wa nchi TAMISEMI amefanya ziara katika shule mbalimbali wilayani Temeke mkoani Dar es Salaam ili kujionea mafanikio yaliyopatikana katika kukabiliana na upungufu wa madawati. https://youtu.be/EFSZUp_OUKw
SIMU.TV: Waziri mkuu Kassim Majaliwa amekutana na mwenyekiti wa kampuni ya ujenzi ya CRCC ya China ambaye ameahidi kushirikiana na serikali katika kuboresha makao makuu ya nchi Dodoma. https://youtu.be/EXF6QqNSYsU
SIMU.TV: Viongozi wa mila wa jamii ya kimasai wameaswa kusuluhisha migogoro ya ardhi pamoja na maeneo ya malisho ili kuondoa athari zinazosababishwa na migogoro hiyo.https://youtu.be/to1l10QkkNA
SIMU.TV: Tanzania inaendesha utafiti wa mbegu mpya za mahindi zilizobadilishwa vinasaba ili kuwezesha zao hilo kuhimili hali ya ukame. https://youtu.be/8dRajuXwddc
SIMU.TV: Serikali ya mapinduzi Zanzibar imesema inahakikisha visiwa hivyo vinajulikana kote duniani kutokana na kilimo na uzalishaji wa viungo. https://youtu.be/3N4629f6TFM
SIMU.TV: Wakala wa usajili wa biashara na leseni BRELA umetoa muda wa miezi miwili kwa wafanyabiashara wanaotumia majina ya biashara kuyasajili. https://youtu.be/rW0u9Pgjvfc
SIMU.TV: Klabu ya soka ya Simba ipo jijini Mbeya ikitarajiwa kushuka uwanjani jumatano hii kucheza na wenyeji wa mkoa huo Mbeya city. https://youtu.be/KQCrisrvUUo
SIMU.TV: Pambano la ngumi la uzito wa juu kati ya bondia mtanzania Ibrahim Klass na bondia kutoka Afrika Kusini linatarajiwa kupigwa katika ukumbi wa Diamond jubilee tarehe 28.https://youtu.be/NYEphMJu1a0
SIMU.TV: Timu ya JKT Mlale imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Polisi Moro kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza. https://youtu.be/TcJuNvNOTkY
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...