Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu amezindua kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa kuweka huduma ya intaneti kwa njia ya Wi-Fi katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu katika jiji la Dar es salaam ili kuongeza fursa kwa watanzania kutumia mawasiliano kwa manufaa ya Taifa katika kuleta maendeleo.

Mheshimiwa Samia Suluhu alizindua huduma hiyo ya W-Fi katika viwanja vya Gymkhana katika uzinduzi wa Kampeni ya kupanda miti iliyofanyika jijini la Dar es salaam Oktoba mosi mwaka huu.

Akizungumza na wakazi waliojitokeza katika viwanja vya Gymkhana, Makamu wa Rais alisisitiza wakazi wa Dar es salaam kupanda miti na kuitunza ili kuhifadhi mazingira hususani katika kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, pia alipongeza juhudi za uwekaji wa huduma ya intaneti kwenye maeneo ya jiji la Dar es salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema kuwa huduma ya Wi-Fi ambayo itawekwa katika maeneo ya mkusanyiko ni sehemu ya juhudi za serikali ya awamu ya Tano kuhakikisha jiji linakuwa na huduma endelevu ya intaneti ambapo wananchi wataweza kupata huduma hiyo popote walipo, kutumia mawasiliano katika kujenga Taifa letu kimaendeleo na kupashana habari mbalimbali za kimaendeleo.

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba alisema kuwa kutokana na uwezo na uzoefu katika sekta ya mawasiliano TTCL iko mstari wa mbele katika kuchangia juhudi za serikali katika kuboresha huduma za TEHAMA kwa kuwafikia watanzania wengi zaidi kupitia huduma hii ya Wi-Fi itakayopatikana katika bustani za mapumziko jijini Dar Es Salaam.

Pia, Kindamba alisema kuwa “Jitihada hizi kwa kushirikiana na wadau wetu mbalimbali zitaendelea na kuhakikisha kuwa sehemu nyingi zenye mikusanyiko ya watu wengi wanapata huduma hii ya Wi-Fi. Mathalani maeneo ya haya ni vituo vikubwa vya mabasi, viwanja vya ndege, vyuo, majengo makubwa yenye wakazi wengi, viunga vya mapumziko, viwanja vya mpira kwa kuwa dunia ya leo mawasiliano ni chachu muhimu katika kuboresha maisha yetu, na kupashana habari na matukio muhimu” Aidha, mpango huu wa Wi-Fi utakua endelevu kufikia lengo la kujenga miji na majiji yetu kwa kiwango cha “Smart City” ili pia kuimarisha ulinzi na usalama wa miji, watu na mali zao.

 Mkuu wa Kanda Kibiashara wa Dar es salaam wa TTCL, Jane Mwakalebela   na wadau  wakipanda miti katika viwanja vya Ghymkhana, Dar e salaam.



   Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu, Bw Waziri Waziri Kindamba akiwa pamoja na wanafunzi wa Skauti, viwanja vya Ghymkhana 



    Wafanyakazi wa TTCL  wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema, baada zoezi la kupanda kukamilika katika viwanja vya Ghymkhana. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akijiunga na mtandao kwa njia ya Wi-Fi kwenye eneo la Gymkhana ambalo huduma ya intaneti ya Wi-Fi inapatikana bure kwa wakazi wa jiji Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Sophia Mjema akishiriki zoezi la kutumia Wi-Fi katika banda la TTCL , ambapo TTCL ilikuwa ikitoa huduma ya intaneti Bure.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw Waziri Waziri Kindamba na Afisa Mkuu wa Masoko na Mauzo, Peter Ngota wakipanda miti katika viwanja vya Ghymkhana, ambapo TTCL iliweka huduma ya intaneti bure  ya Wi-Fi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...