Mkuu wa Kitengo cha uhusiano na Uhamasishaji cha SSRA, Bi. Sarah Kibonde Msika
akifafanua jambo alipokuwa akitoa mada ya Hifadhi ya Jamii katika kongamano la
huduma za Fedha lililoandaliwa na Kampuni ya Mikono Speakers hivi karibuni.
Mgeni rasmi katika maonesho ya huduma za kifedha Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustine Kamuzora akipata maelezo kuhusu shughuli za Mamlaka kutoka kwa Afisa wa SSRA, Ally Masaninga, Maonesho yaliyoandaliwa na Kampuni ya Mikono Speakers katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau walioshiriki wakisikiliza mada ya Hifadhi ya Jamii toka kwa Mkuu wa Kitengo
cha Uhusiano na Uhamasishaji kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii
(SSRA), katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii
(SSRA), wakitoa maelezo na huduma zinazofanywa na Mamlaka katika ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es Salaam, sambamba na Kongamano lililokuwa likifanyika katika ukumbi wa huo, hivi karibuni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...