Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.



Baada ya ushindi wa jana wa goli 1-0 dhidi ya  Tanzania Prisons, kikosi cha Azam kwa sasa kinaondoka kwenda visiwani Zanzibar kujiandaa na mivhuano ya Mapinnduzi inayotarajiwa Desemba 31 huku benchi jipya la ufundi likijizatiti kufanya vizuri kwenye mashindano hayo.

Katika mchezo huo wa ligi kuu ulikuwa ni wa mwisho kwa Azam  kabla ya kuukaribisha mwaka mpya ‘2017’,  na bao pekee la ushindi likiwekwa kimiani na nahodha John Bocco ‘Adebayor’, katika dakika ya 40 baada ya kupokea pasi safi ya Joseph Mahundi na kuwahadaa mabeki wa Prisons kisha kupiga shuti la kiufundi lililojaa kimiani.

Azam FC iliingia kwenye mchezo huo ikiwa na sura mpya kwenye benchi la ufundi lililosimamiwa na makocha wa timu yake ya vijana, Idd Nassor Cheche na Idd Abubakar na hii ni kufuatia kuwasitishia mikabata wakufunzi kutoka Hispania wakiongozwa na Kocha Mkuu, Zeben Hernandez na h

uo ni ushindi wa kwanza wa Azam FC kwenye mechi za mzunguko wa pili wa ligi baada ya kuanza vibaya kwa kutoka sare mechi mbili mfululizo dhidi ya African Lyon (0-0) na Majimaji (1-1).


Kocha Iddy Nassor Cheche amesema kuwa, kwa sasa anachokiangalia ni kuweza kuisaidia timu yake kuweza kufanya vizuri kwenye kombe la Mapinduzi na si vinginevyo na zaidi ana imani na kikosi che kwani kinaweza kufanya vizuri ya mchezo wao dhidi ya Prison.

Azam FC kwa sasa inaelekea kwenye changamoto nyingine ya kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambapo itaanza kufungua dimba Jumatatu ijayo kwa kucheza na Zimamoto saa 10.15 jioni ndani ya Uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar wakipangwa katika kundi moja na mabingwa watetezi wa ligi kuu Yanga huku mechi yao ikitarajiwa kuwa Januari 06.

Kiungo wa Azam Fc Joseph Mahundi akijaribu kumtoka beki wa Prison katika mchezo uliofanyika jana usiku kwenye  Uwanja wa Azam Complex Chamazi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...