EFM redio imejinyakulia tuzo NNE usiku wa kuamkia jana katika tuzo za Tanzania Leadership Awards (T.L.A 2016) kwa vipengele vya Redio bora ya mwaka, Kampuni bora kwa ubunifu, kampuni inayokua kwa kasi pamoja na tuzo ya mwandishi bora ya mwaka ambayo imekwenda kwa mtangazaji wa kipindi cha uhondo katika redio hiyo bibie Dina Marios.
Hafla ya ugawaji tuzo hizo ilifanyika  siku ya tarehe 27/1/2017 katika ukumbi wa Hyatt regency hotel jijini Dar es salaam, ambapo redio hiyo iliwapatia heshima kubwa wasikilizaji wake kwa kuondoka na tuzo hizo.
Ni mwaka wa pili mfululizo kwa redio hio kuchukua tuzo za Tanzania Leadership Awards ambapo tuzo ya kwanza waliipata mwaka jana kwa kipengele cha redio bora ya mwaka.
Ni takribani miaka mitatu sasa tangu redio hii ianzishwe na imejipatia umaarufu mkubwa kwa kuutangaza muziki wa singeli, na kujihusisha na mambo mbalimbali ya kijamii kupitia matamasha,vipindi na kampeni mbalimbali kama vile kupanda miti (mti wangu), kuanzisha vikundi vya mazoezi (efm Jogging club), kampeni za afya, kuhamasisha jamii kujikita katika shughuli za ujasiliamali, pia kutatua matatizo katika jamii  kwa lengo la kujiweka karibu na jamii nzima .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...