Na Antony John ,Globu ya Jamii

TASISI inayoshughulika na uandaaji wa Semina na Makongamano ya Mafunzo ya kazi kwa vitendo ya Guru Plane, imeandaa Semina ya kuwajengea uwezo vijana walio hitimu vyuo vikuu pamoja na vyuo mbalimbali ilikuepukana na tatizola ajira nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mkurugenzi mtendaji wa tasisi hiyo Nickosn Magezi amesema Vijana wengi ukumbwa na kizingiti cha changamoto ya uzoefu wa kazi wanapoingia katika soko la ajira.

Magezi amesema utafiti unaonyesha vijana wengi wanao hitimu vyuo vikuu na vyuo vingine Nchini wanakumbana na changamoto za kutopata ajira kutokana sababu ambazo zimekuwa zikitumiwa na waajiri wengini ni suala la wahitimu kukosa uzoefu wa kazi.

“ Semina hii itakuwana lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kuwapatia uzoefu wahitimu wa vyuo mbalimbali kwa mafunzo ya vitendo hilo ndio lengo kubwa ya semina yetu” amesema Magezi.

Sanjari na hayo ameongeza kuwa semina ya mafunzo ya kazi kwa vitendo imeweza kutatua changamoto za ukosefu wa ajira hasa pale taasisi na makampuni zinapokuwa zimehakikishiwa uzoefu wa kazi unaoendana na soko la ajira.
Mkurugenzi wa guru plane Nickosn Magezi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...