KATIKA kusherehekea msimu wa sikukuu za Krismas na Mwaka mpya, uongozi wa Jengo la biashara la Mlimani City kwa kushirikiana na wafanyabiashara waliopo ndani yake, waliandaa promosheni maalum kwa wateja waliofika kununua bidhaa mbalimbali kwenye maduka yaliyomo ndani ya Jengo hilo, ambapo droo yake imechezeshwa leo na mshindi wake ameondoka na gari mpya aina ya Renault Kwid yenye thamani ya Dola za marekani elfu nane miatano (8,500). Pichani ni Mgeni rasmi katika hafla hiyo, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Edwin Rutageruka aliemuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Adelhelm Meru, akichanganya vikaratasi wakati wa droo ya kumtafuta mshindi wa gari mpya aina ta Renault Kwid, iliyofanyika mchana wa leo ndani ya Mlimani city, Jijini Dar es salaam. Mshindi wa Gari hilo ametambulika kwa jina la Julius Lyanga aliefanya manunuzi katika duka la Game.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Edwin Rutageruka akipokea mfano wa funguo ya gari aina ya Renault Kwid kwa niaba ya mshindi, kutoka kwa Meneja Mkuu wa Jengo la Biashara la Mlimani City, Pastory Mrosso.
Sehemu ya wadau walioshiriki na gari iliyoshindaniwa.
"Huyu ndie mshindi wetu leo"
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...