Na  Bashir  Yakub.

Wakati  mwingine  ununuzi  wa  ardhi   huweza  kuchukua  muda. Hii  ni  kutokana  na  mazingira ya ardhi  yenyewe  inayouzwa  au  kununuliwa  inavyokuwa.  Wakati  ununuzi  unachukua  muda  pia  huweza   kuchukua  gharama.  Gharama  hizi  zaweza  kuwa  zinatolewa na  mtu    anayetaka  kununua  au  anayetaka  kuuza.

Ifahamike  mapema kuwa  ardhi  hapa  tunazungumzia  viwanja, nyumba na  majengo.
Swali  letu  litakuwa ni je gharama  hizi  zinalindwaje na  sheria  ili  mtu  asiingize  gharama  halafu   kuuziwa  akauziwa  mtu  mwingine. Kabla  ya  hilo hapa  chini tuzijue  gharama  zinazoweza  kuingizwa  kabla  ya  kununua. 

1.  GHARAMA   KABLA  YA KUNUNUA  ARDHI.
( i )   Mnunuzi  katika  kutaka  kujiridhisha   kama  muuzaji  kweli  ni  mmliki   halali na  ikiwa ardhi  haina  mgogoro  hutakiwa  kufanya  upekuzi  maalum( official search).  Upekuzi  huu  hufanyika  ardhi  na  huwa  ni gharama . Ada  lazima  ilipwe  kabla  ya  upekuzi.

( ii )   Gharama  za  mwanasheria. Kwasababu  ununuzi  ni  mchakato  wa  kisheria  basi wanunuzi  huwaingiza  wanasheria katika  mchakato  huu   tangu  anapoiona  ardhi, kuipenda  na  kutangaza  kuinunua  kutoka  kwa  mmiliki. Kwasababu  mwanasheria  atampa  ushauri  wa  awali,  atamwandalia  maombi  ya  upekuzi,  atamsaidia  kukagua  hati  miliki na  mengine mengi, basi  gharama  za  awali  kabla  ya  mkataba  wa  ununuzi lazima  hutolewa.

( iii )  Wengine huwasaidia  wauzaji   katika  gharama  za mchakato  wa  kuteuliwa  kusimamia  mirathi  ili  waweze  kuwauzia ,  na  wengine  huwasaidia  wauzaji  kuwalipia  madeni  ili  ardhi  iwe  huru  na  iweze  kununulika.  

( iv )  Gharama  nyingine  huhusisha  upekuzi ( official  search)  BRELA  iwapo  mchakato  unahusisha  kampuni  mbili  au  hata  moja.  Hutakiwa  kulipia  ada  BRELA  ili  waweze  kukupatia  taarifa  za uhai,  ufu,   au  hadhi  ya  kampuni  kwa  muda  huo.

Gharama zote hizi  na  nyingine  nyingi  hutolewa  na mnunuzi  mtarajiwa  kwa  kutegemea ahadi   aliyopewa  na  muuzaji   kuwa  atamuuzia  yeye  na  si  vinginevyo.

2.  HATARI (RISKS)  YA  KUTOA  GHARAMA   KABLA.
Unaweza  kuwa  umetoa  gharama  hizi  ukiamini  kabisa   kuwa  baada  ya  kila  kitu  kwenda  vizuri   wewe  ndiye  utakayeuziwa  hiyo  ardhi.  Badala yake   muuzaji  akapata   mtu  mwingine  mwenye   ofa  kubwa   akakukwepa  na  kumuuzia  huyo  mtu.

Wakati  huu  hatajali  gharama  ulizokwisha  ingiza  katika  mchakato  wala  muda mwingi  uliopoteza  katika  kufuatilia  mchakato.  Ni  katika  mazingira haya   ambapo  mnunuzi  hutakiwa  kulindwa  na  mkataba  maalum  kabla  hajanunua  ardhi.


KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...