Mradi umeandaliwa na AMREF shirika lisilo la kiserikali,umezinduliwa Wilayani Handeni katika ukumbi wa Kanisa la KKT na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe. Kuzinduliwa kwa mradi huo kumekuja Kufuatiwa kuwepo kwa jamii nyingi za wafugaji na jamii nyingine za kawaida zinazodumisha Mila potofu ya ukeketaji wa watoto na wanawake bila kutambua athari wanazokumbana nazo walengwa. Tathmini iliyofanyika imeonesha Asilimia 70% ya wafugaji wanafanya ukeketaji na 30% ni jamii ya kawaida ambayo inadumisha mila hizo.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Mhe. Gondwe alisema kuwa jamii hazikatazwi kudumisha mila na kufanya sherehe za kimila, lakini serikali na jamii kwa ujumla haitakuwa tayari kuona tamaduni potofu kama ya Ukeketaji inaendelea kukumbatiwa na kuathiri watoto na wanawake wa Wilaya Handeni.”

Aliongeza kuwa Vitendo vya ukeketaji vinamuathiri mtoto kisaikolojia ,kiafya, kiuchumi na Kielimu, hali inayopelekea utoro uliokithiri shuleni na watoto wengi kutomaliza shule na kuolewa katika umri mdogo , kutokana na mazingira wanayojengewa na mangariba wakiwa kwenye sherehe hizo za kiutamaduni.

Mhe. Gondwe alieleza kuwa mradi huu ambao AMREF wameuleta kwetu tuna wajibu wa kuumiliki, kuufanya wa kwetu na endelevu hata baada ya mwaka mmoja kufika ukomo . Alieleza kuwa Kila mtoto anahaki ya kuishi na kupata haki zake za msingi ikiwemo elimu kama mtoto mwingine na kwamba jamii nzima ya Handeni iungane na kutoa ushirikiano kuanzia ngazi ya vitongoji hadi Halmashauri kwa shirika la AMREF kuondokana na vitendo hivyo kutoka 14% iliyopo sasa hadi 0%.

Akielezea muundo mzima wa mradi huo, Dokta Aisha Bianaku Meneja wa Mradi alisema kuwa, Mradi huo wameamua kuuleta Handeni baada ya kufanya tahmini na kuona kwamba katika mkoa wa Tanga ikitoka wilaya ya Kilindi, Handeni ni wilaya inayofuata kwa kushiriki vitendo hivi vya ukeketaji. Alisema kuwa kata tano ndizo zitakazopewa elimu na kutoa njia mbadala kwa mangariba ambao wamechukulia kukeketa ni njia mojawapo ya wao ya kujipatia kipato.

Elimu itatolewa kuanzia shuleni kwa waalimu na wanafunzi, mitaani , kwa viongozi wa kata na vitongoji, matabibu wa vituo vya afya, morani na wazee wenye ushawishi mkubwa katika jamii. 

Alisema kuwa lengo ni kuwaelimisha madhara ya vitendo vya ukeketaji na kuondoa kabisa desturi hii ambayo inamadhara makubwa ya kiafya na kielimu kwa ujumla kwa watoto na wanawake hasa wakati wa kujifungua. Akaongeza kuwa AMREF imeona ni vyema kutumia jamii zetu kuleta mabadiliko katika jamii.

Mradi huu umedhaminiwa na mdhamini anayejulikana kwa jina la Sternstunden chini ya shirika la AMREF GERMAN ili kuongezea nguvu mradi wa kupinga ukeketaji ambao kwa awamu ya kwanza utafanyika kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Januari 1/2017 hadi Desemba 31/2017. Kata zitakazonufaika na mradi huu kutokana na tathimini ya uwepo wa jamii ya wafugaji wengi na kukithiri kwa tamaduni hii ya ukeketaji ni pamoja na Segera, Malezi, Konje, Kwamagome na Ndolwa ambapo kiasi cha uro 176,634.22 sawa na milioni miatatu za kitanzania zitatumika kutekeleza mradi huo.

Alda Sadango
Afisa Habari
Halmashauri ya Wilaya Handeni.
  Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe akizungumza na wakuu wataalamu wa Wilaya ya Handeni wakati wa uzinduzi huo.
  Baadhi ya wataalamu wa Wilaya ya Handeni walioshiriki uzinduzi huo.

 Kamati ya ulinzi na usalama  wakimsikiliza  Mhe. Mkuu wa Wilaya kwenye ufunguzi wa mradi huo.
Daktari Aisha Bianaku ambaye pia ni mratibu wa mradi  akiwaelezea wataalamu kuhusu mradi na mikakati iliyowekwa kuwafikia walengwa.
Bw. Henry Bendera mwezeshaji wa mradi kutoka AMREF akizungumza wakati wa uzinduzi huo. 
 Daktari Sarafina Mkua Mratibu wa afya ya uzazi kwa mama na mtoto AMREF kitaifa akielezea baadhi ya athari za ukeketaji. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Habari, Nilikuwa nafuatilia huu mradi wa ukeketaji. Ni mradi mzuri sana na hongereni kwa kuubuni.
    Huu mradi mpaka sasa elimu yake au semina yake inatolewa kwa lugha za KIGENI hivyo kutowafikia walengwa wote. Sielewi kwanini hizi programm hazifanyiki kwa lugha ya kiswahili ambayo ndo lugha ya walengwa.Moja ya sababu hizi elimu haziwafikii walengwa ni lugha inayotumika kuwaelimisha watu kuanzia ngazi ya juu mpaka ya chini. Tubadilike ili tuweze kuwaelimisha watu wasiojua kingereza, ili tuweze kuwaelimisha wasiojua kingereza wawaelimishe wasiojua kingereza. Lets Swahili OWN this.
    asanteni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...