Na Rose Msoka, Zanzibar
Wananchi wa Zanzibar leo wamejitokeza kwa wingi kwenye sherehe za uzinduzi wa maonesho ya sherehe za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yanayoendelea kwenye viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
Maonesho hayo yamezinduliwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa  Dr. Ali Mohamed Shein, ambaye pamoja na mambo mengine amesisitiza Taasisi za Serikali na binafsi kutumia vema fursa ya maonesho kujitangaza na kuonyesha shughuli wanazofanya kwa wananchi.
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ni miongoni mwa Taasisi zinazoshiriki maonesho hayo ambapo pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa Vitambulisho, inaendesha zoezi la kusajili wananchi ambao bado hawajasajiliwa, kugawa vitambulisho vya Taifa kwa wananchi waliokamilisha taratibu za usajili, pamoja na kuonesha mfumo salama (tovuti) inayotumika kusoma taarifa za mtu zilizoko kwenye mfumo kwa njia ya mtandao. Njia hiyo itawezesha wadau mbalimbali kutumia mfumo huo kuhakiki taarifa za mwananchi mwenye kitambulisho kabla ya kumpatia huduma.
Banda la NIDA limekuwa moja ya mabanda ya kuvutia, ambapo wananchi wengi  wamekuwa wakitembelea shughuli mbalimbali zinazoendelea kwenye viwanja hivyo na kuonekana kuridhishwa na huduma zinazotolewa na NIDA.
Maonesho ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yameanza tangu Jumamosi tarehe 07 Januari 2017 yakihusisha Taasisi mbalimbali za Serikali zikiwemo Taasisi za Muungano, mashirika na Taasisi binafsi na yanatarajiwa kumaliza Jumamosi tarehe 14/01/2017.
 Wafanyakazi  wa NIDA wakiwa katika picha ya pamoja katika Banda lao la  maonyesho katika viwanja vya maonyesho vya Biashara vya Maisara Zanzibar  tayari kuhudumia wananchi watakaohudhuria.
 ) Ofisa wa NIDA  Ng Abdulaziz Juma Mtumwa akimkabidhi Dada Lidia Adminic Kaguo Kitambulisho chake katika Banda la Maonyesho wakati maonesho ya sherehe za Mapinduzi Zanzibar yakiendelea kwenye  viwanja vya  Maisara
 
 Kaimu Meneja  wa kitengo cha Operesheni Zanzibar Ndg. Abdallah O. Mmanga akitoa elimu juu ya matumizi ya Vitambulisho Vya Taifa kwa wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Maonyesho vya Maisara Zanzibar
 
 Bi.  Shau Mwalim Haji akimsajili mwananchi aliejitokeza katika maonyesho ya Biashara ya Maisara.
Wananchi wakijisajili kwenye kitabu cha wageni walipofika kutembelea banda la Maonesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) viwanja vya Maisara Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...