Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali wakati alipowasili katika viwanja vya Ukumbi wa zamani wa baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja leo katika semina ya Siku moja kuhusu Umuhimu wa Takwimu na matumizi yake.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akifungua semina ya siku moja kuhusu Umuhimu wa Takwimu na Utekelezaji wake kwa Viongozi mbali mbali katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mnazi Mmoja leo,(kushoto) Makamo wa Rais Balozi Seif Ali Iddi na katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Kiongozi Dkt.Abduhamid yahya Mzee (kulia).
Mtakwimu Mkuu wa Serikali Bibi Mayasa Mahfoudh Mwinyi alipokuwa akitoa Muhtasari wa Majukumu ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali katika Upatikanaji wa Takwimu na Utekelezaji wake katika semina ya viongozi iliyofanyika leo katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Mjini Unguja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...