Tangu kuingia madarakani kwa awamu ya tano ya uongozi wa nchi yetu, msisitizo mkubwa umewekwa katika kutekeleza ahadi ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge. 
Kwa kulitambua hilo mwaka wa fedha 2015/2016 Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) ilianza maandalizi ya Ujenzi wa reli mpya ya standard gauge kwa kuanza kuandaa makabrasha ya zabuni za kuwaajiri mkandarasi wa ujenzi wa reli ya kati pamoja na mshauri mwelekezi mnamo mwezi Mei, 2016 na hatimae, Zabuni ilitangazwa tarehe 9 Septemba, 2016 kwa kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro na tarehe ya kurudisha zabuni ilikuwa 6 Disemba, 2016.
Wakandarasi 40 walinunua zabuni na baada ya tathmini ya zabuni, Ubia (JV) kati ya YAPI MERKEZİ İNŞAAT VE SANAYI A.Ş.  (Uturuki) MOTA-ENGIL, ENGENHARIA E na CONSTRUÇÃO ÁFRICA, S.A. (Ureno) ilionekana kukidhi vigezo vya kiufundi na kifedha.Timu ya watalaamu ilitumwa kutembelea miradi aliyopata kuitekeleza huko nchini Uturuki, Ethiopia, Falme za Kiarabu, Msumbiji na Afrika Kusini na kujiridhisha. Baada ya majadiliano yaliyofanyika kati ya tarehe 21 january, 2017 mpaka 2 Februari 2017 hatimaye maafikiano ya mkataba yalifikiwa kufanya ujenzi kama kama ifuatavyo:-
  1. Kilometa 205 za njia kuu na Kilomita 95 za njia za kupishania treni na maeneo ya kupangia mabehewa jumla kilometa 300, kwa uzani wa tani 35 kwa ekseli,
  2. Ujenzi wa miundimbinu ya umeme, Dar-Morogororo na kwenye njia za kupishania na kupangia mabehewa ya treni,
  3. kiwango cha mwendo kasi wa treni kuwa kilomita 160 kwa saa,
  4. Stesheni 6 za abiria na 6 za kupishania treni,
  5. Kujenga wigo wa kilomita 102 kwa usalama wa watu na magari lakini vivuko vitajengwa kwa matumizi ya waenda kwa miguu na magari pamoja na mifugo.
  6. Muda wa mradi ni miezi 30 baada ya kuanza ujenzi,
Leo tarehe 3 Februari, 2017, ikiwa ni miaka 112 tangu reli ya zamani iliyopo ijengwe, serikali ya awamu ya 5 imeamua kujenga reli mpya ya standard gauge kwa mizigo tani milioni 17 kwa mwaka kwa treni ya umeme yenye mwendokasi wa kilometa 160 kwa saa na miundombinu yenye uhimili mkubwa wa tani 35 kwa ekseli. Kwa hakika nchi yetu itasonga mbele kwa kasi na kuvuna uchumi wa kijiografia ilionao.
Leo tunashuhudia utiaji saini makubaliano ya ujenzi wa sehemu ya kipande cha reli ya kati kati ya Dar es Salaam na Morogoro chenye Kilometa 205 kati ya Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli na Ubia (JV) kati ya YAPI MERKEZİ İNŞAAT VE SANAYI A.Ş.  (Uturuki) MOTA-ENGIL, ENGENHARIA E na CONSTRUÇÃO ÁFRICA, S.A. (Ureno). Gharama za mradi zitakua ni dola za kimarekani 1,029,900,000 ukiongeza na kodi ya serikali dola za kimarekani 185,382,000 jumla kuu ni dola za kimarekani 1,215,282,000. Kipande hiki ni sehemu ya kwanza kati ya 5 ambazo zitatekelezwa hadi kufikia mwanza. Sehemu nyingine ambazo zimetangazwa na zabuni zake zitafunguliwa mwezi wanne mwanzoni ni:-

a)      Morogoro hadi Makutopora                336Km            (Sanifu-Jenga)
b)      Makutopora hadi Tabora                     294Km            (Sanifu-Jenga)
c)      Tabora hadi Isaka                                133Km            (Sanifu-Jenga)
d)     Isaka hadi Mwanza                             248Km            (Jenga)

IMETOLEWA NA:
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji,
RAHCO
Dar es Salaam
03 Februari, 2017
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza  wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa (Standard gauge) kutoka Dar es salaam hadi Morogoro unaotarajiwa kuanza hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 Katibu mkuu wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano (sekta ya uchukuzi) Dkt. Leonard Chamuriho akizungumza  katika hafla ya utiaji saini ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa (Standard gauge) kutoka Dar es salaam hadi Morogoro unaotarajiwa kuanza hivi karibuni
 Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu Mhe.Profesa Richard Sigalla akizungumza  katika hafla ya utiaji saini ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa (Standard gauge) kutoka Dar es salaam hadi Morogoro unaotarajiwa kuanza hivi karibuni
 Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,Masanja Kadogosa kwa kushirikina na Meneja wa Kanda ya Africa Mashariki,Murat Hasim na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Motaengil Africa,Manuel Antonio, wakisani  mkataba wa ujenzi wa reli ya kiwango cha kimataifa (Standard gauge) kutoka Dar es salaam hadi Morogoro unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Bw. Masanja Kadogosa (kulia) na Meneja wa Kanda ya Africa Mashariki, Murat Hasim na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Motaengil Africa,Manuel Antonio wakibadilishana  mikataba hiyo
 Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Bw. Masanja Kadogosa (kulia) na Meneja wa Kanda ya Africa Mashariki, Murat Hasim na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Motaengil Africa,Manuel Antonio wakiinyanyua juu mikataba hiyo. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...