Teresia Mhagama na Zuena Msuya, Arusha
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na Mbunge wa Simanjiro, James Millya wametembelea Kituo cha Jimolojia Arusha, unapofanyika Mnada wa Pili wa Kimataifa kwa madini ya Tanzanite ili kujionea jinsi mnada husika unavyoendeshwa.
Mnada huo wa kimataifa unaofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 9 hadi 12, Februari, 2017 unahudhuriwa na wanunuzi mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi na wauzaji kutoka ndani ya nchi.
Akitoa maelezo kuhusu  mnada huo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini katika Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo, alisema kuwa lengo la mnada huo ni kuhakikisha kuwa madini ya Tanzanite yanapata soko rasmi na Serikali kupata mapato yake stahiki.
 Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almasi na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo,(wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (wa Tatu kushoto) na Mbunge wa Simanjiro, James Millya (wa kwanza kulia) mara walipotembelea Kituo cha Jimolojia Arusha unapofanyika Mnada wa Pili wa Kimataifa kwa madini ya Tanzanite ili kujionea jinsi unavyoendeshwa.Wa kwanza kushoto ni mmoja wa wakurugenzi wa Mgodi wa Tanzanite One, Faisal Shahbhai. 
 Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na Watumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini wakiangalia jinsi wanafunzi katika Kituo cha Jimolojia jijini Arusha wanavyojifunza namna ya kukata madini ya vito na kuyaweka katika maumbo ya kuvutia. Kituo hicho cha Jimolojia kipo chini ya Wizara ya Nishati na Madini.
 Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almasi na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo,(wa kwanza kushoto) akitoa maelezo kwa Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na Watumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Kituo cha Jimolojia jijini Arusha ambacho kipo chini ya Wizara ya Nishati na Madini.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (katikati) akizungumza na mmoja wa wanunuzi wa madini ya Tanzanite katika Mnada wa Pili wa Kimataifa wa Madini hayo unaofanyika jijini Arusha. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almasi na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo na wa kwanza kulia ni mmoja wa wakurugenzi wa Mgodi wa Tanzanite One, Faisal Shahbhai.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almasi na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT) Archard Kalugendo, (katikati)  akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na Mbunge wa Simanjiro, James Millya (wa kwanza kulia) waliotembelea mnada wa Pili wa  Kimataifa wa Madini ya Tanzanite jijini Arusha. Wajumbe hao ni Mhe. John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini (CHADEMA), (wa kwanza kushoto), Mhe. Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum (CCM),(wa pili kushoto),  ) na Mhe. Dunstan  Kitandula Mbunge wa Mkinga (CCM) (wa pili kulia). Wengine katika picha ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini, Adam Juma (wa Tatu kulia) na Kaimu Mratibu wa Kituo cha Jimolojia cha Arusha, Erick Mpesa (wan ne kulia). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...