Wakazi wa jiji la Mwanza wamezifurahia simu za kisasa za Smart Bomba ambazo zilizinduliwa na kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania hivi karibuni,Simu hizo zinazidi kuchangamkiwa na wananchi wengi hususani wakazi wa maeneo ya jiji la Mwanza na wanaozunguka mkoa huo ambapo wameshukuru kwa hatua hiyo ambayo imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya mawasiliano nchini.
Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati wa promosheni ya mauzo ya simu hizo inayoendelea mkoani Mwanza,baadhi ya wananchi wamesema kuwa hatua ya kampuni hiyo kuingiza sokoni simu za kisasa za Smart Bomba zinazopatikana kwa gharama nafuu imedhihirisha dhamira ya kweli ya kampuni hiyo ya kuwapeleka watanzania katika ulimwengu wa kidijitali.
Bw.Focus Phabian mmoja wa wananchi ambaye amenunua simu hiyo akiongea kwa niaba ya wenzake alisema kuwa Smart Phone ni mkombozi wa mawasiliano ya kisasa kwa kuwa licha ya kuwa na unafuu wa bei pia imetengenezwa kwa kuendana sambamba na mazingira halisi ya watanzania.
Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya Ziwa ,Ayubu Kalufya akiitambulisha simu ya Smart Bomba kwa wakazi wa jijini Mwanza jana, kulia ni Mkuu wa Maduka ya Rejareja wa kampuni hiyo,Brigite Steven. 
Baahi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania kanda ya Ziwa wakiandamana kwenye barabara ya Kenyatta jiji Mwanza jana, wakati wa kuitambulisha wa simu aina ya Smart Bomba kwa wakazi wa jiji hilo jana.
Mkazi wa Nyasaka mkoani Mwanza Michael Alfred, akipokea simu
aina ya Smart Bomba ikiwa ni zawadi kutoka kwa Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya ziwa ,Ayubu Kalufya,baada ya kununua moja ya simu hizo wakati wa kuzitambulisha simu hizo jijini Mwanza.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...