Halmashauri ya Wilaya ya Handeni imepokea mbegu za mhogo, mahindi na viazi lishe katika kuhamasisha kilimo cha mazao yanayostahimili ukame na kuboresha kiwango cha elimu kwa kuwapatia chakula wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Mbegu hizo zilizotolewa na shirika lisilo la kiserikali la World Vision kwa Tarafa za Mkumburu na Kwamsisi katika wilaya ya Handeni mkoani Tanga na zitasambazwa kwa shule 20 za msingi na nne za sekondari zikiwa ni juhudi za shirika hilo kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha kilimo cha mazao yanayovumilia ukame na kuboresha kiwango cha elimu kwa kuwapatia chakula wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Akipokea mbegu hizo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe alilishukuru shirika la World Vision kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya Wilaya ya Handeni za kuhamasisha kilimo cha mazao yanayoendana na mabadiliko ya tabia nchi. 

“Mbegu hizi zitakuwa mfano kwa watu wa Handeni na kubadilisha fikra za wakulima kwa kulima mazao yanayovumilia ukame ili kuendana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo ilikuwa kampeni kubwa ya wilaya ya Handeni ya kuhamasisha watu kulima zao la mhogo, viazi na mazao mengine yanayostahimili ukame” alisisitiza Gondwe.

Aliongeza kuwa mbegu hizo zitasaidia kupata chakula kwa wanafunzi na kusaidia kuboresha afya na kuinua kiwango cha taaluma. “Mashamba yatakayolimwa mbegu hizi yatakuwa mfano bora kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya shule. Halmashauri itaweka mfumo mzuri ambao utakuwa utakuwa ni mkataba baina ya Mkurugenzi na walimu wakuu na wakuu wa shule kuonesha kuwa wanawajibu wa kuhakikisha mbegu hizo zinakuwa” alisema Gondwe. 
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe (wa kwanza kushoto) pamoja na  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe wakipokea mbegu za mahindi ya njano kutoka kwa Msimamizi wa mradi Bw. Kelvin Metta wa World Vision.
  Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondweakiwa ameshikilia mbegu za miche ya Viazi, kushoto ni Mkurugenzi  Mtendaji, kulia Kaimu Afisa kilimo Bi. Rosemary Bughe,Wakuu wa Shule  na Maafisa ugani  wakipata maelekezo mafupi kuhusu mbegu.
Kaimu Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bi. Rosemary Bughe  akiwa ameshikilia kifurushi kimojawapo cha mbegu za miche ya mihogo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...