Mkurugenzi wa Msama Promotions,Alex Msama akizungumza mbele ya waandishi wa habari mapema leo mchana jijini Dar kuhusiana na maendeleo ya maandalizi ya tamasha la pasaka linatlotajia kuanza hivi karibuni.


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.

Tamasha kubwa la muziki wa injili linalofahamika kama "Tamasha la Pasaka" sasa kufanyika katika uwanja wa Uhuru april 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mratibu wa Tamasha hilo, Alex Msama amesema kuwa maandalizi yote yamekamilika na sasa uwanja wa uhuru ndio sehemu maalum ya kufanyia Tamasha hilo.

“Malengo ya tamasha la pasaka ni yaleyale ni kuliombea taifa na kumuombea Rais wa nchi Dkt John Pombe Magufuli  ili aendelee kutawala kwa amani katika taifa hili” amesema

Ametaja kuwa tamasha hilo kwa sasa litatembea katika mikoa kumi na kufanya uzinduzi wa albamu mbili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...