Kampuni inayojihusisha na Ufumbuzi mawasiliano ya teknologia Telkom and business Connex imezindua rasmi Mfumo mpya na wa Kisasa unaotumika kurahisisha mawasiliano ya miamala ya biashara na mawasiliano.
Akizunguza na waandishi wa habari Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya ufumbuzi wa mawasiliano ya teknologia Seronga Wangwe amesema Uzinduzi wa BCX unafungua ukurasa mpya katika mwelekeo wa ufanisi wa kibiashara kwa teknologia pevu barani Afrika.
"BCX inaweka bayana aina ya mawasiliano na mahitaji yote ya kampuni yaliyomo barani Afrika katika kutoa ufumbuzi sahihi wa matatizo ya mawasiliano ya kibishara katika masoko yake ya ndani na hatimaye kupenya nje ya mipaka na kisambaa barani kote." amesema Wagwe.
Mkurugenzi mtendaji wa Telkon and Business Connexion(BCX) kushoto Bw Seronga Wangwe akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo,kulia ni Meneja Msaidizi wa Mauzo wa Telkon and Bussnes Connexion (BCX) Bw Ebbenezer Massawe



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...