Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba amesema mchakato wa uanzishwaji wa Chaneli ya Habari za Utalii kuzinduliwa Desemba 20 mwaka huu.
akizungumza wakati wa uwasilishaji wa mada ya Chanel ya Utalii kwa Wahariri na Waandishi wa Habari wakati wa mkutano wa Utalii na Tanzania ya Viwanda ulioandaliwa na TANAPA Jijini Tanga..
"Chanel hii ni moja ya vitu ambavyo vitasaidia katika kukuza utalii wetu hivyo sasa tupo katika mchakato na wabia wetu TANAPA, NGORONGORO na wadau wengien wa masuala ya habari" amesema Dr Rioba .
Amesema kuwa kikubwa wanachokiangalia sasa ni aiana gani ya uwekezaji unatakiwa kufanywa hili kufanya chombo hicho kuwa bora zaidi hili kuweza kumvutia kila mtu .
aidha Dk Rioba ametoa fursa kwa wadau na wanahabari kutoa maoni yao juu ya namna gani Chanel hiyo inapaswa kuwa hili kuvutia.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba akitoa ufafanuzi kuhusu mchakato wa kuanzisha chaneli ya Utalii ndani ya televisheni y Taifa (TBC),mbele ya Wahariri na Waandishi waandamizi mapema jioni ya leo katika katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...