Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan  amezipongeza juhudi zinazofanywa na taasisi ya Merck ambayo ni kampuni inayoongoza katika sayansi na teknolojia  ambayo imelenga  kushughulikia masuala  uwezeshwaji wa wanawake na huduma za afya akisema kwamba wamekuja nchini  kwa wakati mwafaka, 
Wakati wa mkutano maalum kati ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Merck Foundation  Makamu wa Rais  alisema kuwa Merck Foundation  inakaribishwa na serikali inatarajia kushirikiana  na taasisi hiyo  inayoheshimika na iliyo makani katika  kuwezesha wanwake , vijana, huduma za afya  na sayansi. 
Tunatambua mchango  unaotolewa na Merck Foundation  katika kujengea uwezo  huduma za afya barani Afrika na tunakaribisha shughuli zake  nchini Tanzania, hususani katika kampeni zinazolenga  kuuongezea umma  uelewa kuhusu ugumba. 
Makamu wa Rais aliongeza, “Mimi binafsi nitafanya kazi na Merck katika kuwawezesha wanawake walio na uwezo duni kijamii na kiuchumi kote nchini Tanzania  na sehemu nyingine duniani ili kujenga utamaduni mpya  katika kuheshimu na kumtambua wanawake  kama sehemu ya wanajamii wanaozalisha  wawe ni kinamama na hata wasio wazazi.” 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha Ofisa Mkuu Mtendaji wa Merck Foundation, Dk Rasha Kelej,  ofisini kwake Ikulu jijini Dar es salaam.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Ofisa Mkuu Mtendaji wa Merck Foundation, Dk Rasha Kelej,  ofisini kwake Ikulu jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...