Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani amesema kuanzia Agosti 30 mwaka huu, Serikali itatangaza zabuni ya kuanza ujenzi wa Mradi Mkubwa wa Umeme wa megawati 2100 katika maporomoko ya maji ya Mto Rufiji mkoani Pwani  eneo la Stiegel’s Gorge
Akizungumza jijini Dar es Salaam Dkt. Kalemani  amesema,  taratibu za awali zimeshaanza ambapo wataalaumu  wa ndani na nje wameshakutana na kuchagua sehemu za kujenga mradi huo katika Mto Rufiji, ambapo tayari Shirika la Umeme Nchini ( Tanesco ) limeanza upembuzi yakinifu wa kujenga miundombinu ya umeme na Wakala wa barabara nchini  (Tanroad) kujenga miundombinu ya  barabara.
Ujenzi wa mradi wa umeme wa megawati 2100 kutoka maporoko ya maji ya Mto Rufiji Mkoani Pwani ( Stiegler’s Gorge)unatarajiwa kuanza ndani ya kipindi cha  miezi miwili ijayo baada ya taratibu za zabuni kukamilika, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani amewambia watanzania kuwa, tayari Serikali imetenga fedha za kutekeleza mradi huo, na hatua za awali za utekelezaji zimekwisha fanyika, ambapo tarehe 30 ya mwezi  huu wa Agosti Serikali itatangaza zabuni kwa wakandarasi wa ndani na nje ya nchi ili waweze kuomba kufanya kazi .
Dkt. Kalemani amesema mkandarasi atakayepewa kazi ya kujenga mradi huo ni yule tu atayeridhia kujenga kwa gharama nafuu na kwa muda mfupi zaidi ya uliowekwa Pia Dkt. Kalemani anatoa ufafanuzi namna ambavyo Serikali imejiandaa katika kutekeleza mradi huo.
Kwa mujibu wa Dkt Kalemani, mradi huo utakapokalimilika utakasaidia kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme nchini  na kwamba Serikali haitarajii kuongeza bei ya umeme. 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dk. Medard Kalemani akishuka kwenye boti kwa ajili ya kuelekea kwenye eneo la Stieglers Gorge kutakapojengwa mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...