Na Agness Moshi na Bushiri Matenda –MAELEZO.

Watanzania na wadau  mbalimbali wa sekta ya Afya nchini wameombwa kuendelea  kuisaidia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ili iendelee kufanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora. 

Hayo yamesemwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe.Tulia Akson, wakati akikabidhi msaada  runinga nne na katoni mbili za maziwa vyenye thamani ya  shilingi 1,000,000 vilivyotolewa kwa watoto waliopo kwenye  Taasisi hiyo kwa  ushirikiano na Dstv, TSN na Kampuni ya Twincity.
 Dkt.Tulia amesema msaada  wa runinga unatimiza ahadi waliohaidi kwa taasisi hiyo na unamaana kubwa sana kwa sababu utawasaidia watoto wanaokaa hospitalini hapo kwa muda mrefu  kujifunza ,na kuwaburudisha  kwa kipindi chote cha matibabu ya awali  kabla ya kufanyiwa upasuaji.
“Watoto hawa wanakaa muda mrefu hospitalini wakitibiwa hivyo wanashindwa kujumuika na wenzao kwa michezo jambo ambalo linawafanya wahisi upweke  kwa kuwapatia runinga kutawasaidia kuondoa hali hiyo , kuwaburudisha na kuwapa nafasi ya  kujifunza kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na king’amuzi cha DSTV”, alisema Dkt.Tulia
 Naye Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt.Mohammed Janabi amesema kuwa si watoto tu watakaofaidika kwani hata wazazi wao wataweza kujua mambo mbalimbali  yanayoendelea Nchini kwa kuangalia taarifa za Habari zitakazokua zinaonyeshwa kupitia chaneli mbalimbali. 
 “ Sio watoto wote wanaokuja hapa wanatatizo la moyo peke yake wengine wanakuja wakiwa na Magonjwa mengine  ambapo inabidi  tuanze kuwatibia kwanza magonjwa hayo ambapo wakati mwingine yanachukua muda mrefu  hivyo basi kwa kipindi chote hicho runinga hizi zitakua zikiwapa burudani, elimu kwa masomo mbalimbali kama vile kiingereza, hesabu  kwa watoto wakubwa na kwa wale wadogo wataburudika kupitia katuni”,alisema Dkt.Janabi.
 Dkt.Janabi ameongeza kuwa msaada wa maziwa waliopewa utasaidia kuimarisha afya za watoto wadogo wanaotibiwa kwani wapo wengine wamekuja wakiwa na Afya duni ,wengine wana magonjwa ya utapia mlo hivyo kupelekea kuchelewa kupatiwa matibabu.
Aidha,Dkt.Janabi amemshukuru Dkt.Tulia kupitia Mfuko wake wa Tulia Trust kwa kuendelea kuhamasisha wadau mbalimbali kuipatia misaada Taasisi hiyo. 
 Kwa upande wake mtoto Mwamvita Hassani mwenye umri wa miaka 13 kutoka wilayani Kondoa kwa niaba ya watoto wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo ametoa shukrani zake kwa Naibu Spika na wadau waliowapa misaada hiyo.“Ninawashukuru sana kwakutuletea Tv na Maziwa,Tumefurahi na tunawaombea watuletee Tv zingine”, alisema Mwamvita.
Dkt.Janabi  amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia upatikanaji wa vitanda kwa ajili ya Taasisi hiyo kwani wanakabiliwa na  changamoto mbalimbali ikiwemo swala la upungufu wa vitanda kwa wagonjwa kwani wanavitanda 128 tu ambavyo havikidhi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika kwa ajili ya matibabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...