Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba kesho ataongoza mkutano wa siku moja utakaozungumzia suala la wakimbizi raia wa Burundi ikiwemo maandalizi ya kuwarejesha kwao wakimbizi raia wa nchi hiyo waliojiandikisha kwa hiari kurejea nyumbani.

Mkutano huo utakaofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam utahudhuriwa na nchi za Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi (UNHCR). 

Mkutano huo unafanyika kwa mujibu wa matakwa ya Sheria za kimataifa zinazohusu wakimbizi ambazo zinazilazimu pande tatu katika suala hilo kukutana na kukubaliana kuhusu namna ya kuwarejesha wakimbizi hao waliohiari kurejea nyumbani.

Katika mnasaba huo, makubaliano ya mkutano huo yataipa fursa kwa upande mmoja Serikali ya Burundi kuingia katika makambi ya wakimbizi kuhamasisha kurejea nyumbani na kwa upande wa pili yatawapa fursa wakimbizi kupitia wawakilishi wao kutembelea Burundi kuangalia hali halisi ili kujiridhisha kabla ya kurudi nchini humo.

Baada ya hatua hizo kukamilika, imeelezwa kuwa Jumuiya ya Kimataifa itatekeleza jukumu lake la kuwarudisha wakimbizi hao nyumbani kwa ‘heshima’ ambapo chini ya utaratibu huo wa ‘heshima’, Jumuiya hiyo itapaswa kuwawezesha wakimbizi hao kuanza maisha mara wanaporejea ikiwemo huduma za chakula na makaazi kwa wale ambao makaazi yao yatakuwa yameathirika.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...