Wakala wa wauzaji wa Vifaa Vya kuunganishia mabomba yanayotoka nchini Marekani, David Robert Mwamsojo akionyesha waandishi wa habari moja ya kiunganishi cha mabomba yanayotengenezwa na kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani katika mkutano wa kuitambulisha kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani iliyoleta nchini Tanzania teknolojia mpya ambayo itasaidia kuokoa miundo mbinu ya maji. Pembeni ni Makamu wa Rais wa Kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani iliyokuja kuwekeza nchini Tanzania katika sekta ya viwanda. Picha na Kajunason/MMG.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Godfrey Simbeye akitoa shukrani zake za pekee kwa kampuni ya GroovJoint iliyokuja nchini Tanzania kuwekeza upande wa viunganishi vya mabomba ambapo alisema kuwa wameamua kuwapokea kwa mikono miwili kampuni hiyo kwa vile viunganishi vitasaidia wananchi kupata maji safi na salama. Pembeni ni Makamu wa Rais wa Kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani iliyokuja kuwekeza nchini Tanzania katika sekta ya viwanda na Wakala wa wauzaji wa Vifaa Vya kuunganishia mabomba yanayotoka nchini Marekani, David Robert Mwamsojo. Makamu wa Rais wa Kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani, David Newman iliyokuja kuwekeza nchini Tanzania katika sekta ya viwanda kwa kuleta viunganishi vya mabomba.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Godfrey Simbeye akimshukuru Makamu wa Rais wa Kampuni ya GroovJoint ya nchini Marekani, David Newman mara baada ya mkutano na waandishi wa habari kuelezea malengo ya kampuni yao. Pembeni ni Wakala wa wauzaji wa Vifaa Vya kuunganishia mabomba yanayotoka nchini Marekani, David Robert Mwamsojo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...