Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa
kushirikiana na Umoja wa Ulaya imekamilisha ujenzi wa Makumbusho mapya ya Olduvai
ambayo yanaonesha Chimbuko
la Binadamu (The Cradle of Humankind)
katika Bara la Afrika.
Makumbusho hayo mapya pamoja na Onesho la Chimbuko la Binadamu, yatafunguliwa
rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tarehe 03 Oktoba,
2017 katika eneo la Olduvai, ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Onesho hilo ni matokeo ya utafiti wa muda mrefu uliofanyika katika Bonde
la Olduvai na Laetoli katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. Wananchi,
viongozi mbalimbali wa kitaifa na Mabalozi wanatarajiwa kuhudhuria kwenye hafla
hiyo.
Idadi kubwa ya vioneshwa
katika Makumbusho hiyo, vilipatikana katika bonde la Olduvai na Laetoli nchini Tanzania
kupitia utafiti wa kisayansi wa muda mrefu na vilikuwa vimehifadhiwa katika Makumbusho
ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Vioneshwa hivi ni pamoja na masalia ya
zamadamu, zana za mawe na masalia ya wanyama walioishi takribani miaka milioni 4
iliyopita.
Makumbusho hayo yamepangwa
kuonesha sehemu kuu nne zinazowiana. Sehemu
ya kwanza inahusu ushahidi wa nyayo
za zamadamu zilizongunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dr. Mary D.
Leakey. Nyayo hizi ziliachwa na zamadamu
anayeiitwa Australopithecus afarensis na
ndio ushaidi usiopingika wa zamadamu kutembea wima kwa miguu miwili takribani
miaka milioni 3.6 iliyopita.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani Morogoro kuhusu uzinduzi wa Makumbusho Mapya ya Olduvai na Onesho la Chimbuko la Mwanadamu ambayo yatazinduliwa tarehe 03 Oktoba, 2017 na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olduvai wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani Morogoro kuhusu uzinduzi wa Makumbusho Mapya ya Olduvai na Onesho la Chimbuko la Mwanadamu ambayo yatazinduliwa tarehe 03 Oktoba, 2017 na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olduvai wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. (Picha na Hamza Temba - WMU)
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...