Na Humphrey Shao
Msanii wa Muziki wa Asili nchini anayetamba katika majukwaa ya kimataifa Msafiri Zawose amewataka watanzania wazidi kumpigia kura hilo aweze kutwaa tuzo ya Afrima katika kipengele cha Muziki wa asili
Zawose ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa Michuzi blog juu ya Mipango yake ya kufanya matamasha nje ya nchi.
"Cha kwanza ni kuwataka watanzania waingie katika website ya afrima kisha kipita katika kipengele cha best tradional music na kumchagua Msafiri Zawose kutoka Tanzania hili niwe mshindi na kuleta heshima kwa taifa" amesema Zawose.
Ametaja kuwa mafanikio makubwa uanzia Nyumbani hivyo ni wakati wa Watanzania kumuunga mkono katika kutambulisha utamaduni wetu kimataifa.
Ametaja kuwa huu ndio muda wa kuweza kuionyesha Dunia namna tulivyojaliwa vitu vya asili ambavyo vinaweza kuwavutia watalii kuja nchinini.
Zawose amemaliza kwa kusisitiza kuwa ni vyema kila mmoja kimpigia kura kadri awezavyo hilo awe kuibuka mshindi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...